Baraza la Madiwani la Manispaa ya Geita limempongeza Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Yefred Myenzi, kwa mafanikio makubwa ya kuongeza makusanyo ya mapato ya ndani kutoka Sh bilioni 14 hadi Sh bilioni 19 ndani ya mwaka mmoja wa uongozi wake.
Pongezi hizo zimetolewa leo Mei 13, 2025, katika kikao cha robo ya nne ya baraza hilo lililoanza kazi mwaka 2020 na kuhitimisha kazi yake Mei 2025 .
Mbali na pongezi hizo kikao hicho pia kilijadili mafanikio mengine yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wao.
Akizungumza kwenye kikao hicho, Meya wa Manispaa ya Geita, Constantine Morandi, alisema mafanikio hayo yametokana na usimamizi madhubuti wa mifumo ya ukusanyaji mapato uliosimamia na Mkurugenzi.
“Ongezeko la Sh bilioni tano kwa mwaka mmoja ni jambo kubwa. Vyanzo vya mapato ni vilevile, lakini mapato yameongezeka. Hii inaonyesha wazi kuwa Mkurugenzi amesimamia vizuri ukusanyaji mapato hatujaongeza vyanzo vya mapato ni vilevile lakini kunaongezeko la Sh Bilion tano,” amesema Morand.
Ameongeza kuwa Mkurugenzi Myenzi amekuwa mfano wa kuigwa kwa uwajibikaji na utendaji bora uliosaidia kuleta maendeleo katika Manispaa hiyo.
Katika kipindi cha miaka mitano, mapato ya ndani ya halmashauri hiyo yameongezeka kutoka Sh bilioni 8 mwaka 2020 hadi kufikia Sh bilioni 19 mwaka huu.
Mafanikio mengine yaliyoelezwa na Meya huyo ni pamoja na ujenzi wa shule mpya, vyumba vya madarasa zaidi ya 400, matundu ya vyoo zaidi ya 420, na maabara mpya 16 kwa shule za msingi na sekondari.
Katika sekta ya afya, vituo vya afya vimeongezeka kutoka kimoja mwaka 2020 hadi kufikia vitano – vinne vikiwa tayari vimekamilika na kimoja kikiwa hatua za mwisho za ujenzi.
Aidha, mikopo kwa wanawake, vijana na makundi maalum kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani imeongezeka kutoka Sh milioni 698 mwaka 2020 hadi kufikia Sh bilioni 1.78 mwaka huu.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Yefred Myenzi amesema zaidi ya Sh bilioni 3 zilitolewa na Serikali Kuu kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka kwa ajili ya miradi mbalimbali ya madeleo.
Amesema matumizi ya fedha hizo ni pamoja na utekelezaji wa miradi ya TASAF, Mfuko wa Jimbo na ujenzi wa kituo cha ualimu kinachojengwa katika kata ya Kalangalala
Ameeleza pia kuwa Manispaa hiyo inaendelea kutekeleza miradi ya CSR yenye thamani ya Sh milioni 422, ambapo Sh milioni 204 tayari zimepokelewa na miradi 18 kati ya 34 imekamilika.
Kuhusu mitihani ya kidato cha sita, Myenzi amesema jumla ya watahiniwa 934 wamesajiliwa, wakiwemo 61 wa kujitegemea, na hadi sasa hakuna changamoto yoyote iliyojitokeza.
Kuhusu hali ya chakula aamesema tathmini ya chakula kwa sasa inaonesha hali ni shwari, hakuna dalili za njaa, huku ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi ukitarajiwa kuanza mwezi Juni baada ya mkandarasi kusaini mkataba.
Akigusia afya ya jamii, Mkurugenzi huyo ameeleza kuwa wagonjwa 30 walibainika kuwa na vimelea vya ugonjwa wa Ipox, ambapo 29 wamepona na watatu wanaendelea na matibabu.
Myenzi amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari.
MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA
TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
Instagram
Geita Tanzania
Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita
Namba ya Simu: 0282520437
Mobile:
Barua pepe: td@geitatc.go.tz
Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa