Mafunzo kwa vikundi vinavyotarajiwa kupewa Mkopo wa 10% ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu yameendelea leo tarehe 09 Mei, 2025 katika ukumbi wa Gedeco katika Halmashauri ya Manispaa ya Geita.
Mafunzo hayo endelevu yameanza kutolewa tangu Jumatano tarehe 07 Mei, 2025 ambayo yanaratibiwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii yenye lengo la kuwaelimisha juu ya usimamizi na uendeshaji miradi yenye tija ili waweze kurejesha fedha za mikopo waliyopewa.
Afisa Vijana wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita, Ndg. Zengo Polle amewasisitiza wanufaika wa mikopo hiyo kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuhakikisha wanaongeza kipato na kurejesha kwa wakati ili wananchi wengine wapate fursa hiyo.
Nao baadhi ya wanufaika wa mafunzo hayo, wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa hiyo ya mikopo. Pia, wameishukuru Halmashauri kwa mafunzo hayo ambayo yatawaongezea ujuzi na usimamizi katika miradi yao ambapo utawasaidia katika urejeshaji wa mikopo hiyo.
Mafunzo haya yameendelea kutolewa katika vituo vinne vya Kalangalala, Mtakuja, Ihanamilo na Kasamwa ambapo wajasiriamali wamewekwa katika vituo ili kuwa na ukaribu wa kufika katika mafunzo hayo ambayo pia yamejumuisha wataalam kutoka TAKUKURU, SIDO, Jeshi la Polisi, Maafisa kutoka idara za Biashara, Viwanda na Biashara, Fedha, Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
Halmashauri ya Manispaa ya Geita kwa robo hii ya tatu ya mwaka wa fedha 2024/2025 imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 1,232,715,000 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu.
TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
Instagram
Geita Tanzania
Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita
Namba ya Simu: 0282520437
Mobile:
Barua pepe: td@geitatc.go.tz
Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa