• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Nyuki na Misitu
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Madiwani Geita Mji Wafanya Ziara Ya Mafunzo Chalinze

Posted on: February 16th, 2023

Madiwani Geita Mji Wafanya Ziara Ya Mafunzo Chalinze

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Geita wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Costantine Morandi, baadhi ya wataalam, wawakilishi wa wakulima pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Cornel Magembe wametembelea Halmashauri za Wilaya ya Chalinze, Mvomero na Halmashauri ya jiji la Tanga kwa lengo la kujifunza mbinu bora na mikakati ya kuboresha ukusanyaji mapato.

Wakiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze mkoani Pwani hivi karibuni ujumbe wa Madiwani kutoka Halmashauri ya Mji Geita wametembelea mradi wa kuzalisha kokoto ambao unamilikiwa na Halmahauri hiyo, ambapo walijifunza namna Halmashauri ya Chalinze ilivyofanikiwa kudhibiti upotevu wa mapato kwa kufunga kamera kwenye vizuizi(Barriers) na desturi ya kuwabadilisha vituo vya kazi wakusanyaji mapato mara kwa mara.

Katika ziara yao waliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro, Waheshimiwa Madiwani walipata fursa ya kutembelea mradi wa Machinjio ya mifugo na Ushirika wa wakulima wadogo wadogo kilimo cha umwagiliaji mpunga Dakawa(UWAWAKUDA LTD) ambapo walitembelea shamba lao na kujifunza namna kilimo cha umwagiliaji kilivyoweza kuwainua kiuchumi wanaumoja hao.

Mwenyekiti wa Bodi ya UWAWAKUDA Ndg. Joseph Lutango ameeleza kuwa ushirika wao wenye wanachama 941 ambao una eneo lenye jumla ya hekta 3,225.15 kati ya hizo 2000 zikiwa na miundombinu ya umwagiliaji na zinatumika katika uzalishaji wa mpunga.

Ndg. Joseph Lutango ameeleza kuwa ushirika wao unawapatia faida mbalimbali zikiwemo upatikanaji wa mikopo mikubwa ya zana za kilimo kama vile matrekta na mashine ya kuvunia mpunga(combine harvester), kuchangia katika huduma za jamii kama vile ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi za walimu katika kata ya Dakawa, upatikanaji wa ajira kwa vijana 5000 kutoka katika kata ya Dakawa na maeneo Jirani Pamoja na wanachama kupata uwezo  wa kujikimu kimaisha wao binafsi Pamoja na familia zao.

Ujumbe wa waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Mji Geita wakiwa ziarani katika Halmashauri ya jiji la Tanga walitembelea mradi wa kiwanda cha kuzalisha matofali ambayo yanatengenezwa kwa mchanganyiko wa mchanga, saruji na kokoto nyembamba. Matofali ambayo yanatumika katika ujenzi wa majengo mbalimbali ya Serikali na watu binafsi. Mradi wa matofali umeiwezesha Halmashauri ya jiji la Tanga kuingiza mapato ya Shilingi milioni 176 kwa mwezi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita Pamoja na timu yake wametoa shukrani za dhati kwa viongozi wa maeneo yote ambayo walipata fursa ya kuyatembelea kwa kuwapokea kwa upendo na ukarimu na kuwajengea uzoefu wa miradi mbalimbali ambayo inawaingizia mapato kwa kiasi kikubwa na kuahidi kuyafanyia kazi mazuri yote ambayo wamejifunza katika ziara hiyo ili kupanua wigo wa ukusanyaji mapato ya Halmashauri ya Mji wa Geita.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI February 23, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI July 22, 2022
  • TANGAZO LA KAZI ZA MACHINJIO August 16, 2022
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA GEITA MJI December 02, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Bilioni 9.8 Kutekeleza Miradi Geita Mji Kupitia CSR

    March 22, 2023
  • Wanawake Watakiwa Kuwa Vinara Kupinga Ukatili

    March 10, 2023
  • Geita Gold FC Yazindua Mfumo Wa Usajili Wa Wanachama

    February 23, 2023
  • Madiwani Geita Mji Wafanya Ziara Ya Mafunzo Chalinze

    February 16, 2023
  • Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA MACHINJIO YA KISASA MPOMVU
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa