• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Madiwani Geita Mji Wafanya Ziara Ya Mafunzo Chalinze

Posted on: February 16th, 2023

Madiwani Geita Mji Wafanya Ziara Ya Mafunzo Chalinze

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Geita wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Costantine Morandi, baadhi ya wataalam, wawakilishi wa wakulima pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Cornel Magembe wametembelea Halmashauri za Wilaya ya Chalinze, Mvomero na Halmashauri ya jiji la Tanga kwa lengo la kujifunza mbinu bora na mikakati ya kuboresha ukusanyaji mapato.

Wakiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze mkoani Pwani hivi karibuni ujumbe wa Madiwani kutoka Halmashauri ya Mji Geita wametembelea mradi wa kuzalisha kokoto ambao unamilikiwa na Halmahauri hiyo, ambapo walijifunza namna Halmashauri ya Chalinze ilivyofanikiwa kudhibiti upotevu wa mapato kwa kufunga kamera kwenye vizuizi(Barriers) na desturi ya kuwabadilisha vituo vya kazi wakusanyaji mapato mara kwa mara.

Katika ziara yao waliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro, Waheshimiwa Madiwani walipata fursa ya kutembelea mradi wa Machinjio ya mifugo na Ushirika wa wakulima wadogo wadogo kilimo cha umwagiliaji mpunga Dakawa(UWAWAKUDA LTD) ambapo walitembelea shamba lao na kujifunza namna kilimo cha umwagiliaji kilivyoweza kuwainua kiuchumi wanaumoja hao.

Mwenyekiti wa Bodi ya UWAWAKUDA Ndg. Joseph Lutango ameeleza kuwa ushirika wao wenye wanachama 941 ambao una eneo lenye jumla ya hekta 3,225.15 kati ya hizo 2000 zikiwa na miundombinu ya umwagiliaji na zinatumika katika uzalishaji wa mpunga.

Ndg. Joseph Lutango ameeleza kuwa ushirika wao unawapatia faida mbalimbali zikiwemo upatikanaji wa mikopo mikubwa ya zana za kilimo kama vile matrekta na mashine ya kuvunia mpunga(combine harvester), kuchangia katika huduma za jamii kama vile ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi za walimu katika kata ya Dakawa, upatikanaji wa ajira kwa vijana 5000 kutoka katika kata ya Dakawa na maeneo Jirani Pamoja na wanachama kupata uwezo  wa kujikimu kimaisha wao binafsi Pamoja na familia zao.

Ujumbe wa waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Mji Geita wakiwa ziarani katika Halmashauri ya jiji la Tanga walitembelea mradi wa kiwanda cha kuzalisha matofali ambayo yanatengenezwa kwa mchanganyiko wa mchanga, saruji na kokoto nyembamba. Matofali ambayo yanatumika katika ujenzi wa majengo mbalimbali ya Serikali na watu binafsi. Mradi wa matofali umeiwezesha Halmashauri ya jiji la Tanga kuingiza mapato ya Shilingi milioni 176 kwa mwezi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita Pamoja na timu yake wametoa shukrani za dhati kwa viongozi wa maeneo yote ambayo walipata fursa ya kuyatembelea kwa kuwapokea kwa upendo na ukarimu na kuwajengea uzoefu wa miradi mbalimbali ambayo inawaingizia mapato kwa kiasi kikubwa na kuahidi kuyafanyia kazi mazuri yote ambayo wamejifunza katika ziara hiyo ili kupanua wigo wa ukusanyaji mapato ya Halmashauri ya Mji wa Geita.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa