• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

MAADHIMISHO YA SIKU YA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

Posted on: January 31st, 2025

Leo tarehe 31 Januari, 2025 Halmashauri ya Manispaa ya Geita imefanya madhimisho ya siku ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele. Maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Uwanja iliyopo katika Kata ya Nyankumbu

Maadhimisho haya uadhinishwa tarehe 30 Januari kila mwaka ili kutilia mkazo udhibiti wa magonjwa haya pamoja na kuhamasisha jamii namna ya kujikinga na kupambana nayo.

Kauli mbiu ya mwaka huu inasema "Tuungane, Tuchukue  hatua, Tutokomeze Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele." Maadhimisho haya yanalenga kuhamasisha katika ngazi za Halmashauri na wadau katika ngazi zote kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha na kuelimisha jamii.

Magonjwa hayo ambayo yanadhibitiwa na mpango wa kitaifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ni pamoja na kichocho, minyoo tumbo, trakoma, usubi, matende na mabusha. Magonjwa haya yamo ndani ya jamii hasa jamii masikini lakini hayakuwa yanapewa umuhimu stahili kama ilivyo kwa magonjwa mengine kama vile Malaria, UKIMWI na mengineyo

Mpango wa kitaifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ulianza mwaka 2008 baada ya mikakati mbalimbali inayotumika kudhibiti magonjwa haya kuingizwa kwenye mpango kabambe wa wizara ya afya.

Dhumuni kuu la mpango huu ni kupunguza maradhi yatokanayo na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele nchini ili kufikisha kiwango ambacho si tatizo katika jamii na mwaka 2012 Wizara ya Afya ilizindua mpango mkakati kwa ajili ya kudhibiti magonjwa haya.

Halmashauri ya Manispaa ya Geita imekuwa ikitekeleza shughuli mbalimbali dhidi ya kukabiliana na magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele kama vile; kutoa dawa za kinga tiba kwa watoto wote wenye umri wa kwenda shule, kutoa elimu kwenye jamii na ujezi wa vyoo. Inakadiriwa watu zaidi ya bilion moja duniani kote tayar wameathirika na watu zaidi ya bilioni mbili walikuwa kwenye hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa hayo.

Kwa kipindi cha mwaka 2024, Halmashauri ya Manispaa ya Geita ilikuwa na jumla ya walengwa 128,974 wenye umri wa kuanzia miaka 5 hadi 14 waliokuwa wameandikishwa shuleni na Halmashauri ilifanikiwa kutoa dawa za kinga tiba za minyoo tumbo kwa shule 97 za msingi na shule 32 za sekondari ambapo jumla ya wanafunzi 127,078 walimeza dawa za minyoo tumbo sawa na 98.52% ya  walengwa wote na wanafunzi waliomeza dawa za kinga tiba za kichocho 84,604 ambao ni sawa na 96.53% ya walengwa 87,645 wote kutoka kwenye Kata ambazo zina maambukizi makubwa ya kichocho

Dkt. Sunday Mwakyusa, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ambaye ni mgeni rasmi amesema kuwa mikakati iliyopo ni kuhakikisha  kuwafikia walengwa zaidi ya 100%

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Geita Dkt. Sunday Mwakyusa akizungumza jambo katika maadhimisho hayo

Maadhimisho haya yamehudhuriwa na maafisa mbalimbali kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Geita pamoja na Walimu na viongozi wa Kata na Mitaa, ambapo burudani mbalimbali zilitolewa pamoja na zoezi la utoaji wa dawa za kinga tiba za minyoo tumbo

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Geita Dkt. Sunday Mwakyusa akifafanua jambo katika maadhimisho hayo


Afisa Elimu Vifaa na Takwimu Shule za Msingi katika Manispaa ya Geita Ndg. Kapela Kahamba akiwa katika maadhimisho hayo


Afisa Lishe wa Manispaa ya Geita Ndg. Matovu Muhihi akitoa elimu ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele katika maadhimisho hayo


Afisa Elimu Watu Wazima katika Manispaa ya Geita Bi. Rahel Mwera akifafanua jambo katika maadhimisho hayo


Mmoja wa wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Uwanja akipata dawa tiba kinga ya Minyoo tumbo katika maadhimisho hayo


Afisa Elimu Kata ya Nyankumbu Ndg. James Magela akifuatilia maadhimisho hayo


Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTD) Bi. Masau Fulano akifuatilia maadhimisho hayo


Baadhi ya Wanafunzi wakifuatilia maadhimisho ya siku ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele


Baadhi ya Wanafunzi wakifuatilia maadhimisho ya siku ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele


Wanafunzi wakitoa burudani katika maadhimisho ya siku ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele


Wanafunzi wakifurahia kupata elimu na vidonge vya tiba kinga ya minyoo ya tumbo katika maadhimisho ya siku ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa