• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Kamati Ya Siasa Wilaya Yakoshwa na Ubora wa Miradi

Posted on: August 24th, 2023

Kamati ya Siasa Wilaya Yakoshwa na Ubora wa Miradi

Wajumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Geita ikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Barnabas Mapande wameridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Mji Geita.

Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati hiyo kukagua utekelezaji wa Ilani hivi karibuni, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Geita ameishukuru Serikali ya Awamu ya sita chini ya jemedari Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuipatia fedha Halmashauri ya Mji Geita, fedha ambazo zimetekeleza na zinaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Mama Samia Suluhu Hassan ana dhamira ya dhati katika kuhakikisha watanzania wanapata huduma muhimu za msingi katika Zahanati zenye viwango, shule bora za Msingi na Sekondari, Hudumay a maji safi na salama Pamoja na Barabara zinazopitika wakati wote. Hivyo wasimamizi kwa ngazi ya Halmashauri msaidieni Mhe. Rais ili nia yake iweze kutekelezeka kikamilifu na kwa usahihi kwa sababu mmepokea fedha nyingi ili kujenga miradi yenye “. Aliongeza Mhe. Mapande.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa wamefurahishwa na maboresho ya elimu ya awali yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya sita kupitia mradi wa uboreshaji wa Elimu ya Awali na Msingi(BOOST) ambapo katika Halmashauri ya Mji Geita madarasa ya awali ya mfano yamejengwa kisasa na kuwekewa mabembea ya kuchezea kwa lengo la kumfanya mtoto apende Kwenda shule, jambo ambalo kwa miaka ya nyuma lilikuwa likifanyika katika shule za watu binafsi na zile za taasisi za kidini pekee.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM Wilaya ya Geita Bi. Naomi Fujo amewaasa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambao wameanzisha vikundi vinavyojishughulisha na Kazi mbalimbali za kujiingizia kipato kutokuwa waoga kukopa kwenye taasisi za kifedha ambazo zinatoa mikopo yenye riba nafuu, bali wanatakiwa watumie fursa hizo ili kukuza mitaji yao na kujiongezea kipato kikubwa zaidi ya kile walichonacho.

Miradi iliyotembelewa na Kamati ya Siasa Wilaya ya Geita ni Pamoja na Ujenzi wa mabweni mawili ya wanafunzi katika Shule ya Sekondari Geita, ujenzi wa Zahanati ya Kigoma road, Kikundi cha wanawake cha kukamua mafuta ya alizeti Kanyala, Shule mpya  ya Msingi Chanama, Shule mpya ya Msingi Juhudi na ujenzi wa Barabara za mitaa katika Kata za Kanyala na Bombambili.


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 MKOA WA GEITA July 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI August 18, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI July 22, 2022
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA GEITA MJI December 02, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Serikali Yapongezwa Kwa Kukuza Uwekezaji

    September 28, 2023
  • Geita Mji Yapongezwa Kuvuka Lengo La Upandaji Miti

    September 25, 2023
  • Geita Mji Yasaini Utekelezaji Miradi ya TACTIC

    September 24, 2023
  • Geita Mji Yanufaika na Vifaa vya Michezo

    September 21, 2023
  • Zaidi

Video

ASANTE SERIKALI YA AWAMU YA SITA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa