• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Kamati Ya Siasa Wilaya Ya Geita Yaridhishwa na Miradi Geita Mji

Posted on: January 26th, 2023

Kamati Ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Miradi Geita Mji

Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Geita wameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Geita kwa usimamizi bora wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa zahanati, vyumba vya madarasa na utoaji mikopo isiyo na riba kwa makundi maalum.

Pongezi hizo zimetolewa hivi karibuni wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kipindi cha miezi sita kuanzia Julai 2022 hadi Disemba 2023.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Barnabas Mapande ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wananchi wake na kutoa fedha ambazo zimetumika katika ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa vyumba vipya 71 vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023 na ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum.

‘’ Napenda kutumia fursa hii kuwasihi watendaji wote wa Serikali kuhakikisha mnasimamia matumizi sahihi ya fedha zinazoletwa na Serikali kwa kujenga majengo yenye ubora uliotarajiwa. Kadhalika nawaomba ndugu zangu wa wilaya ya Geita kuendelea kujitolea nguvu kazi katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo Serikali yetu tukufu inatoa fedha  kwa lengo la kuboresha Maisha ya kila mtanzania.” Aliongeza Ndg. Mapande.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM Wilaya ya Geita Bi. Naomi Fujo ameipongeza Serikali kupitia Halmashauri ya Mji wa Geita kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya mkopo kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ambao wanafanya shughuli mbalimbali za kujikwamua kiuchumi. Bi. Naomi amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kufanya kazi kwa bidi na uaminifu ili waweze kufanya marejesho kwa wakati.

Miradi iliyotembelewa na Kamati ya Siasa Wilaya ni pamoja na ujenzi wa madarasa mapya tisa katika Shule ya Sekondari Mkolani, bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum Shule ya Msingi Kasamwa, Zahanati ya Nyakahengele, upanuzi wa chanzo cha maji Nyankanga  na  kutembelea vikundi viwili vilivyonufaika na mikopo isiyo na riba kutoka Halmashauri ya Mji Geita ambavyo ni kikundi cha vijana Maisha Kata ya Nyankumbu ambacho kinajishughulisha na utengenezaji wa mikanda ya Gypsum na Kikundi cha wanawake Tema kinachopatikana katika Kata ya Kalangalala na kinajishughulisha na utengenezaji wa mvinyo wa asili kwa kutumia ndizi mbivu.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa