• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Kamati Ya Lishe Geita Mji Yapata Ujuzi Bukombe

Posted on: September 15th, 2022

Kamati Ya Lishe Geita Mji Yapata Ujuzi Bukombe

Wajumbe wa Kamati ya lishe ya Halmashauri ya Mji wa Geita wakiongozwa na mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Geita Ndugu Janeth Mobe pamoja na wanavikundi viwili vya wanawake na vijana wanaonufaika na mkopo wa asilimia 10 ya mapato ya halmashauri, unaotolewa na Serikali wamefanya ziara ya mafunzo katika eneo la Runzewe Kata ya Uyovu Wilayani Bukombe.

Akizungumza kwa niaba ya wajumbe Ndg. Janeth Mobe amesema kuwa ziara hiyo imefanyika tarehe 14/9/2022 kwa kuwatembelea kikundi cha Bora kilimo-Biashara ambacho kinajishughulisha na uchakataji wa nafaka na uzalishaji wa unga lishe wenye virutubishi vyenye Asidi ya foliki, Vitamin B12, Madini ya chuma na madini ya zinki.

Bi. Mobe ameongeza kuwa ziara hiyo imefanywa baada ya kutambua umuhimu wa Halmashauri ya Mji Geita kujifunza namna ya kuzalisha unga wa mahindi na muhogo wenye mchanganyiko wa madini na vitamini ambao una faida mbalimbali zikiwemo kuzuia upungufu wa damu, kuongeza ukuaji wa mwili na akili, kuongeza ulaji wa vyakula vyenye viini lishe, kuongeza uwezo wa kujifunza na kuelewa pamoja na kuzuia matatizo ya kiafya yatokanayo na upungufu wa vitamin na madini. Hivyo unga huo ni muhimu kwa wanafunzi wa shule za Geita mji ambazo zina hosteli na mabweni.

Kikundi cha Bora-Kilimo Biashara kilianzishwa mwaka 2014 kikiwa na idadi ya wanachama watano ambao ni wahitimu wa vyuo vikuu waliojiunga pamoja na kujikita kwenye masuala ya kilimo na ufugaji ambao walipatiwa sehemu ya mtaji wao na Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe na kufanikiwa kununua mashine moja ya kusaga na baada ya miaka kadhaa walipanua biashara yao kwa kuongeza mashine ya kukoboa mahindi, kukoboa mchele na kuuchambua kulingana na viwango tofauti.

Mpaka sasa kikundi hicho kimefanikiwa kuwa na ofisi mbili na sasa wanajenga mashine ya kukamua alizeti, kutengeneza ajira ya vijana 19 kutoka kwenye maeneo ya mradi wao ambao wanafanya shughuli mbalimbali za kiwandani hapo. Vijana hao pia wamefanikiwa kupata masoko ya bidhaa zao kutoka kwenye shule za bweni, kusafirisha nchi za jirani kama Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi na maeneo mbalimbali nchini Tanzania.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • MKUTANO MAALUMU WA BARAZA WA KUJADILI MAJIBU YA HOJA NA MAPENDEKEZO YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    June 11, 2025
  • BILIONI 19.1 KUTEKELEZA UJENZI KITUO KIKUU CHA MABASI MANISPAA YA GEITA

    June 06, 2025
  • WATUMISHI GEITA MANISPAA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI ZA UTUMISHI WA UMMA

    June 05, 2025
  • WATUMISHI WA MANISPAA YA GEITA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MITANDAO YA KIJAMII YENYE TAARIFA ZA UPOTOSHAJI

    June 04, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa