• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Jamii Yatakiwa Kulipa Kipaumbele Suala la Lishe

Posted on: November 9th, 2023

Jamii Yatakiwa Kulipa Kipaumbele Suala la Lishe

Katibu Tawala wa Wilaya ya Geita Ndugu Lucy Beda ameiasa jamii katika Halmashauri ya Mji Geita kuhakikisha suala mtambuka la lishe linapewa kipaumbele kwa kuwapatia wajawazito, watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano na walioko shule wanapatiwa chakula bora chenye vitamini zote na madini mbalimbali.

Katibu Wilaya ya Geita ameyasema hayo hivi karibuni alipomuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Geita kwenye kikao cha uhamasishaji wa utekelezaji wa mkataba wa lishe kilichofanyika katika ukumbi wa Nyerere EPZ Bombambili Geita mjini kikiwahusisha Madiwani wote wa Halmashauri ya Mji Geita.

Ndg. Lucy Beda amewaasa Waheshimiwa Madiwani kuwa mabalozi wazuri ambao watatumika kufikisha elimu ya lishe kwa jamii na kushirikiana na Mkurugenzi wa Halmashauri katika kuhakikisha Halmashauri haibadili matumizi ya vifungu vya bajeti za lishe kwa ajili ya shughuli nyingine zinazoibuka.

‘’Waheshimiwa Madiwani mna wajibu wa kutetea upatikanaji wa elimu endelevu kuhusu desturi nzuri za ulaji, usindikaji na uhifadhi wa chakula na kuhamasisha matumizi ya vyakula vya asili na vinavyopatikana katika maeneo ya walaji, pia mjitahidi kuwahamasisha wanaume wajihusishe na kushiriki katika upangaji wa namna ya kuboresha desturi za ulaji na lishe kwenye familia zao. ‘’ Aliongeza Ndg. Lucy Beda.

Akizungumza juu ya umuhimu wa jamii kuwekeza kikamilifu katika masuala ya lishe, Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Geita Bw. Matovu Muhihi amesema kuwa lishe duni hudumaza ukuaji wa Watoto kimwili na kiakili na kuathiri ukuaji wa akili unaopelekea kupungua uwezo wa kufanya vizuri shuleni na pia hupunguza ufanisi katika maisha ya utu uzima, kwa hiyo ni muhimu kuwekeza kwenye lishe ili kuwa na jamii ya watu wenye afya nzuri ya mwili na akili wenye uwezo wa kuchangia katika maendeleo ya taifa.

Halmashauri ya Mji Geita kama zilivyo halmashauri nyingine hupimwa utekelezaji wake wa afua mbalimbali za lishe kwa kutumia viashiria vilivyo katika mkataba wa lishe unaotekelezwa katika ngazi ya halmashauri na kata kwa mujibu wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ya Chama Cha Mapinduzi( CCM).

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KOZI YA AWALI YA JESHI LA AKIBA WAPATIWA ELIMU YA HABARI

    July 04, 2025
  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa