• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Jamii Yatakiwa Kuepuka Uharibifu wa Mazingira

Posted on: April 4th, 2023

Jamii Yatakiwa Kuepuka Uharibifu wa Mazingira

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela ameiasa jamii mkoani Geita kuachana na tabia ya kukata miti hovyo kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu kama kilimo, ufugaji, uchomaji mkaa na ukataji miti kwa ajili ya shughuli za uchimbaji madini.

Mkuu wa Mkoa wa Geita ametoa kauli hiyo aliposhiriki katika zoezi la upandaji miti wakati wa maadhimisho ya siku ya upandaji miti kitaifa yaliyofanyika kimkoa katika Kata ya Lulembela wilayani Mbogwe hivi karibuni.

Mhe. Shigela ameagiza kuwa kila familia inatakiwa iweke utaratibu wa kupanda walau miti mitano kila mwaka ili kupendezesha mazingira na kupata faida nyinginezo zitokanazo na miti.

“Ndugu zangu miti ndio kila kitu katika Maisha yetu, tunapata maji kupitia miti, tunategemea miti kupata mvua za uhakika kwa ajili ya kutuwezesha kulima kwa uhakika na kuvuna mazao mengi, tunapata dawa za mitishamba kwa ajili ya kutibu maradhi mbalimbali kutoka kwenye majani, magome, matunda na mizizi ya miti. Hivyo kila mmoja wetu atambue kuwa uharibifu wa mazingira ndio chanzo cha mabadiliko ya tabia ya nchi na tusipokuwa makini mabadiliko hayo yatagharimu vizazi vyetu vijavyo kwa kiasi kikubwa Zaidi kuliko hali ilivyo kwa sasa.” Aliongeza Mhe. Shigela.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mhe. Costantine Morandi amewataka wananchi kutimiza wajibu wa kupanda miti kuanzia ngazi ya familia ili kuirejesha hali ya mkoa wa Geita kama ilivyokuwa miaka ya nyuma ambapo kulikuwa na misitu mikubwa sana lakini sasa hivi watu wamekuwa na desturi ya kukata miti hovyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Ndg. Lee Joshua amesema Serikali inajitahidi kuhamasisha wananchi, taasisi na wadau wote walioko katika mnyororo wa utunzaji mazingira kupanda na kuhifadhi miti lakini mwitikio bado ni mdogo, hivyo viongozi wote wa vijiji, mitaa hadi kata wafanye suala la upandaji miti na uhifadhi wa mazingira kama agenda yao ya kudumu. Kadhalika doria za mara kwa mara ziendelee ili kudhibiti wananchi wanaoharibu misitu kwa makusudi Pamoja na kuendelea kutoa elimu ya utunzaji wa misitu ili kuwa na uelewa wa Pamoja juu ya umuhimu wa kuhifadhi mazingira.

Maadhimisho ya Siku ya upandaji miti kitaifa mwaka 2023 yaliongozwa na kauli mbiu isemayo “Tanzania ya kijani bila miti hakuna uhai” ambayo inahamasisha jamii kuacha kuharibu misitu na kuendelea kupanda miti ili kufikia lengo la upandaji miti kimkoa ambapo kila Halmashauri inatakiwa kupanda miti milioni moja na nusu kwa mwaka, kuanzia Oktoba 2022 hadi sasa Halmashauri ya Mji Geita imeshapanda miti 750,000 sawa na asilimia 50% ya lengo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • DC KOMBA AWAKARIBISHA NACHINGWEA KUJIFUNZA UCHIMBAJI GEITA, ATOA USHAURI WA NAMNA NZURI YA USIMAMIZI WA MIGODI

    June 26, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa