• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Jamii Yashauriwa Kuwapeleka Watoto Kwenye Chanjo

Posted on: April 25th, 2023

Jamii Yashauriwa Kuwapeleka Watoto Kwenye Chanjo

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Cornel Magembe ametoa wito kwa wazazi wa jinsia zote kuhakikisha wanawapeleka Watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kupata chanjo ambazo zitawakinga na kuwalinda dhidi ya maradhi mbalimbali yanayozuilika kwa chanjo.

Mhe. Magembe ametoa kauli hiyo tarehe 24/4/2023 alipokuwa akizungumza na wazazi waliojitokeza kwa wingi katika viwanja vya Zahanati ya Nyankumbu Geita mjini katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya chanjo kwa mkoa wa Geita.

Mkuu wa Wilaya ya Geita ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kujali afya za wananchi wake kwa kutoa fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa, ujenzi wa zahanati na vituo vya kutolea huduma za afya zikiwemo hospitali kubwa Pamoja na kuwezesha kampeni mbalimbali zenye lengo la kuboresha afya za watu.

β€œIli Watoto wetu wanufaike na chanjo, tunao wajibu wa kuwapeleka kwenye kliniki kupitia utaratibu uliopangwa ili wapatiwe chanjo tangu kuzaliwa kwao hadi mtoto anapotimiza umri wa juma 6,10 na 14 pamoja na chanjo ya surua mtoto anapotimiza umri wa mwaka mmoja na nusu. Hivyo ndugu zangu baba na mama tafadhali tutumie fursa hii kuwapeleka Watoto wakachanjwe katika wiki hii ya maadhimisho na baada ya wiki ya chanjo huduma zitaendelea katika vituo vyote vya kutolea huduma ya afya.” Aliongeza Mkuu wa Wilaya ya Geita.

Mratibu wa chanjo Mkoa wa Geita Bi. Wille Luhangija amesema kuwa katika maadhimisho hayo Mkoa wa Geita umelenga kuwafikia Watoto 12,237 wenye umri chini ya miaka mitano waliopo katika ratiba ya chanjo na Watoto 1763 waliopo nyuma ya ratiba ya chanjo na wasichana 9067 wenye umri wa miaka 14 kwa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi ambao wengi wao wapo shuleni.

Bi. Luhangija ameongeza kuwa chanjo zitakazotolewa katika zoezi hilo ni zilezile ambazo hutolewa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya katika ratiba ya kawaida ya utoaji huduma za chanjo. Chanjo hizo ni salama na hutolewa bila malipo yoyote na wataalam wenye ujuzi. Hivyo wazazi wanatakiwa kufuata ratiba ya chanjo kwa Watoto na kuepukana na upotoshwaji kuhusiana na huduma zote za chanjo.

Maadhimisho ya wiki ya chanjo 2023 yamebebwa na kauli mbiu isemayo β€œ Tuwafikie wote kwa chanjo, jamii iliyopata chanjo, jamii yenye afya.”




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa