• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Halmashauri Yatakiwa Kuendelea kutoa Mikopo ya Wanawake

Posted on: March 8th, 2019

Halmashauri Yatakiwa Kuendelea Kutoa Mikopo ya Wanawake

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mheshimiwa Leonard Bugomola ameiagiza Idara ya Maendeleo ya Jamii, Halmashauri ya Mji Geita kuhakikisha  asilimia nne ya mapato ya ndani ya Halmashauri inayotakiwa kutolewa kama mkopo kwa vikundi vya wanawake wanaojishughulisha na kazi mbalimbali za uzalishaji mali zinatolewa kwa wakati.

Mhe. Bugomola ameyasema hayo hivi karibuni wakati wa Maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika katika ngazi ya Halmashauri kwenye viwanja vya soko kuu Geita mjini.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji aliongeza kuwa Serikali inathamini na kutambua jitihada za wanawake katika kujishughulisha na kazi mbalimbali za maendeleo kama ufugaji mifugo, biashara ndogondogo na nyinginezo ambazo zinawawezesha kujikwamua kiuchumi wao binafsi, familia zao na Taifa kwa ujumla. Hivyo kama fedha hizo hazitatolewa kwa wakati zitakwamisha mipango mikakati ya kina mama hao.

Akisoma taarifa ya wanawake wa Mji wa Geita Bi. Rehema Mteta amesema kuwa wanaishukuru Halmashauri ya Mji Geita kwa kuwapatia mikopo katika vipindi tofauti ambapo mikopo hiyo imewawezesha wanawake kuondokana na mfumo dume unaowafanya kina mama kuwa tegemezi kwa waume zao, pia wamekuwa wakichangia pato la Taifa kwa kulipa kodi katika shughuli zao za kiuchumi na idara ya maendeleo ya jamii wamekuwa mstari wa mbele kutoa mafunzo ya  mara kwa mara juu ya elimu ya ujasiriamali na namna ya kuboresha shughuli zao.

Bi. Mteta amebainisha changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni kusubiri mikopo kwa muda mrefu baada ya kuwasilisha fomu za maombi, Baadhi wa wanawake kutorejesha mikopo waliyoichukua kwa wakati ili iweze kutolewa kwa waombaji wengine. Pia kina mama wachache kutokuwa waaminifu na kutokomea na mikopo waliyopatiwa na Halmashauri kwa malengo ya kujiendeleza kiuchumi.

Siku ya wanawake Duniani huadhimishwa tarehe 8 kila mwaka Duniani kote kwa lengo la kutambua jitihada zinazofanywa na wanawake wote katika kujikwamua kiuchumi ambapo kauli mbiu ya mwaka 2019 ni “Badili fikra kufikia usawa wa kijinsia kwa maendeleo endelevu.”



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KOZI YA AWALI YA JESHI LA AKIBA WAPATIWA ELIMU YA HABARI

    July 04, 2025
  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa