• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Halmashauri Yahimizwa Kukamilisha Miundombinu Ya Shule Kwa Wakati

Posted on: July 20th, 2023

Halmashauri Yahimizwa Kukamilisha Miundombinu Ya Shule Kwa Wakati

Viongozi na wataalamu wote wanaosimamia ujenzi wa miundombinu ya madarasa, mabweni na vyoo vya wanafunzi wamesisitizwa kuhakikisha kuwa miundombinu hiyo inayojengwa katika shule za awali, msingi Pamoja na Sekondari kupitia mradi wa BOOST na wafadhili mbalimbali unakamilika kwa wakati ili ianze kutoa huduma kama ilivyokusudiwa

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa( TAMISEMI) Bwana Sospeter Mtwale alipofanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Mji Geita na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni matatu ya wanafunzi katika Shule ya Sekondari Geita ambayo yanajengwa kwa Shilingi Milioni 360 kutoka Serikali kuu na vyumba vinne vya madarasa Pamoja na choo cha wanafunzi vinavyojengwa kwa fedha za huduma ya kampuni kwa jamii kutoka Kampuni ya Barrick Tanzania.

Bw. Mtwale ametoa shukrani kwa kampuni ya Barrick kwa fedha za utekelezaji wa miundombinu hiyo na kuipongeza Halmashauri ya Mji Geita kwa usimamizi mzuri na kueleza kuwa lengo la ziara yake mkoani Geita ni kukagua miundombinu ya elimu inayojengwa na Serikali ya awamu ya sita Pamoja na wafadhili mbalimbali. Pia kuhimiza uwajibikaji na usimamizi wa miradi hiyo kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

“Upanuzi wa miundombinu ya kidato cha tano katika Shule ya Sekondari Geita kupitia fedha za Serikali ukamilike kwa wakati kwa kuzingatia ubora wa thamani ya fedha itakayotumika, kadhalika mafundi wanaojenga majengo hayo wanatakiwa kusimamiwa ipasavyo na wahandisi wa halmashauri katika hatua zote za ujenzi ili kupata majengo yenye ubora na yanayoendana na fedha iliyotolewa.” Aliongeza Bw. Mtwale.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Ndg. Zahara Michuzi amesema amepokea maelekezo hayo na kuahidi kuendelea kushirikiana na wataalamu wengine wakiwemo mafundi wanaojenga miundombinu hiyo kusimamia ujenzi kikamilifu na kuhakikisha wanakamilisha ndani ya wakati uliopangwa ili miundombinu hiyo iweze kuwanufaisha wanafunzi.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa