• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Halmashauri ya Mji Geita Yajipanga kukusanya Bilioni 5

Posted on: March 2nd, 2018

Halmashauri ya Mji Geita Yajipanga kukusanya Bilioni 5 Mwaka 2018/2019

Halmashauri ya Mji Geita  imekisia kukusanya jumla ya Shilingi 5,114,157,735 toka vyanzo vya ndani ambayo fedha hii imejumuishwa katika jumla ya Bajeti  ya mwaka  2018/2019 ambayo ni Shilingi 44,983,794,197.00.

Akiongea wakati wa kikao cha Baraza Maalum la Bajeti  lililoketi Tarehe 01/3/2018 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Geita kwa lengo la kupitisha  bajeti ya Mwaka wa fedha 2018/2019, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Geita Mheshimiwa Leonard Kiganga Bugomola amesema kwa mwaka wa fedha uliopita Halmashauri ilipanga kukusanya zaidi ya Shilingi Bilioni 5, ambapo hadi kufikia mwezi Disemba 2017 Halmashauri imeweza kukusanya kiasi cha Shilingi 2,868,353,850.15 sawa na asilimia 52.

Mh. Bugomola ameongeza kuwa kutokana na mafanikio ya ukusanyaji uliofikia nusu ya makadirio ana imani kuwa mpaka kukamilisha mwaka wa fedha 2017/2018 mwezi Juni mwaka huu, Halmashauri itakuwa imefikisha lengo la makusanyo. Aidha makusanyo  hayo yanatoa mwanga wa mafanikio katika bajeti iliyopitishwa kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Mhandisi Modest Apolinary amesema kuwa Halmashauri inategemea kukusanya mapato yake kutoka kwenye vyanzo mbalimbali kama kodi ya huduma( service levy) kutoka kampuni ya Mgodi wa Dhahabu Geita na Kampuni nyingine zinazofanya kazi na Mgodi huo, kodi ya nyumba za kulala wageni, Leseni za biashara,faini mbalimbali, upigaji chapa mifugo na ushuru wa mifugo, ushuru wa mazao mbalimbali na matunda.

“Katika Bajeti ya mwaka   2018/2019. Jumla ya Shilingi   15,585,248,344 zimetengwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo, Kiasi cha shilingi 24,632,539,165 kwa ajili ya mishahara ya watumishi na Shilingi 4,765,976,688 kwa ajili ya matumizi mengineyo”. Aliongeza Mhandisi  Modest Apolinary.

Katika Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019, Halmashauri ya Mji Geita imejielekeza katika kufikia vipaumbele vyenye shabaha na malengo ambayo ni Kuendelea kuboresha na kuimarisha mfumo wa makusanyo ya mapato ya ndani ili kuongeza  mapato ya Halmashauri, Kuboresha Sekta za huduma za jamii, hususan, Elimu, Afya, Maji, Barabara, Mifugo, Uvuvi, Kilimo, Misitu, Maendeleo ya Jamii, Ushirika,

Kusaidia Sera ya Taifa kufikia Uchumi wa kati wa uendelezaji wa viwanda na  Kuimarisha Utawala bora.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa