• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Mji Yapongezwa Kuvuka Lengo La Upandaji Miti

Posted on: September 25th, 2023

Geita Mji Yapongezwa Kuvuka Lengo la Upandaji Miti

Halmashauri ya Mji Geita imepongezwa kwa kufanikiwa kupanda miti 1,500,451 kwa mwaka 2022/2023 ambayo ni sawa na asilimia 100.03% ya lengo la Taifa.

Pongezi hizo zimetolewa tarehe 25/09/2023 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mheshimiwa Selemani Saidi Jafo alipokuwa akizungumza na wananchi kabla hajazindua zoezi la upandaji miti katika eneo la EPZA Bombambili ambapo Maonesho ya sita ya kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanaendelea.

Mhe. Jafo amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitoa agizo kwa kila Halmashauri kuhakikisha inapanda miti milioni moja na laki tano kwa kila mwaka ambapo Halmashauri ya Mji Geita kwa kushirikiana na wadau mbalimbali zikiwemo Taasisi za Umma na binafsi, Shule za Msingi na Sekondari, wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla wamefanikiwa kupanda miti kwa zaidi ya asilimia 100.

Waziri Jafo amewaagiza wananchi kuendelea kupanda miti kuanzia mitano kwenye makazi yao na sehemu za kazi na kuitunza vyema ili vizazi vijavyo viweze kunufaika na miti iliyopandwa na jamaa zao. Pili kwa kuendelea kupanda miti watatunza mazingira na kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa mjumbe wa Bodi ya Mabadiliko ya Tabianchi.

“Nawaagiza Wakala wa Misitu Tanzania watoe vitalu vya miti vya kutosha ili wananchi wasikose miti ya kupanda na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) watengeneze mkaa mbadala wa kutosha na wabainishe maeneo utakapokuwa unapatikana ili wananchi waupate wakati wote na si kusubiri kipindi cha Maonesho pekee.” Aliongeza Mhe. Jafo.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Ndugu Lee Joshua amesema kuwa mafanikio yaliyopatikana yametokana na uhamasishaji uliofanywa na kitengo ambapo wataalam wa misitu hutembelea mashamba ya wakulima kwenye Shule za Msingi na Sekondari ambapo wanafunzi wana wajibu wa kuhakikisha wanatunza miti waliyopanda. Pia Taasisi mbalimbali na watu binafsi wameendelea kuhamasishwa juu ya umuhimu wa kupanda miti katika maeneo yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • MKUTANO MAALUMU WA BARAZA WA KUJADILI MAJIBU YA HOJA NA MAPENDEKEZO YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    June 11, 2025
  • BILIONI 19.1 KUTEKELEZA UJENZI KITUO KIKUU CHA MABASI MANISPAA YA GEITA

    June 06, 2025
  • WATUMISHI GEITA MANISPAA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI ZA UTUMISHI WA UMMA

    June 05, 2025
  • WATUMISHI WA MANISPAA YA GEITA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MITANDAO YA KIJAMII YENYE TAARIFA ZA UPOTOSHAJI

    June 04, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa