• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Mji Yapitisha Bajeti 2019/2020

Posted on: January 21st, 2019

Geita  Mji Yapitisha Bajeti 2019/2020

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji wa Geita limepitisha makadirio  ya Shilingi 49,312,038,078 katika kutekeleza majukumu mbalimbali ikiwemo  Mishahara, matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2019/2020.

Akiwasilisha mapendekezo ya Bajeti hiyo wakati wa mkutano wa Baraza la Madiwani tarehe 21/01/2019 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mji,  Afisa Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji wa Halmashauri ya Mji wa Geita Bi. Sylvia Rwehabura amesema kuwa Halmashauri ya Mji imeandaa Mpango na Bajeti ya Mwaka 2019/2020 kwa kuzingatia maelekezo ya Mwongozo wa kitaifa wa miaka mitatu, mipango shirikishi ya jamii na vipaumbele vya Halmashauri.

Bi. Rwehabura ameongeza kuwa Halmashauri  ya Mji imezingatia masuala muhimu kama kuimarisha usimamizi wa mapato ya ndani kwa kufanya tathimini na kuibua vyanzo vipya vya mapato, kutumia mifumo ya kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato na kupanga matumizi katika maeneo ya vipaumbele.

Kwa upande wa sekta mbalimbali Halmashauri ya Mji  imejipanga kutenga maeneo ya viwanda, kilimo na mifugo, nyuki,vituo vya kutolea huduma za jamii, kiuchumi na utawala za miundombinu ya afya, maji, elimu, misitu ya jamii, maeneo ya maafa na stendi. Pia kuhakikisha kamati za watu wenye ulemavu, mabaraza ya wazee na kamati za kutokomeza ukatili dhidi ya mtoto na mwanamke zinaanzishwa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mhandisi Modest Apolinary amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2018/2019 katika sekta ya utawala Halmashauri imefanikiwa kuendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa soko la Kalangalala ambalo lina majengo mawili, jengo moja likiwa ni kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo na lina vizimba 108 na jengo la pili ni ghorofa lenye sakafu ya chini na juu kwa ajili ya biashara za kibenki na duka kubwa (supermarket).

Katika mwaka wa fedha 2019/2020 mapato yanayotegemewa kukusanywa na kupokelewa  ni mishahara shilingi 33,690,176,760.31, matumizi ya kawaida ni shilingi 886,895,000, miradi ya maendeleo shilingi 8,084,872,892 na mapato ya ndani ya Halmashauri ni shilingi 6,425,993,950 ambazo zinafanya jumla ya shilingi 49,312,038,078 zinazokadiriwa kutumiwa na Halmashauri ya Mji wa Geita katika kutekeleza majukumu mbalimbali .




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa