• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Mji Yang'ara Makusanyo ya Mapato

Posted on: July 31st, 2018

Geita Mji Yang’ara Ukusanyaji wa Mapato

Halmashauri ya Mji wa Geita imeibuka kidedea kati ya Halmashauri za Miji 22 Tanzania Bara katika ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2017/2018. Halmashauri ya Mji wa Geita imefanikiwa kukusanya jumla ya Shilingi 5,931,976,537.38/= sawa na asilimia 107.57% ambapo malengo ya makusanyo yalikuwa ni Shilingi 5,514,320,052.00/=

Akizungumza wakati wa mahojiano na mwandishi wa habari hii Mwekahazina wa Halmashauri ya Mji wa Geita Ndg. Munguabela Kakulima amesema kuwa sababu zilizopelekea mafanikio makubwa katika ukusanyaji wa mapato ni pamoja na uwazi na matumizi ya mifumo ya kielektroniki ambayo imeongeza Imani na kuziba mianya ya upotevu wa mapato.

Mwekahazina wa Halmashauri ya Mji wa Geita ameongeza kuwa uelewa wa wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kulipa kodi, upatikanaji wa takwimu sahihi juu ya idadi ya walipa kodi, sehemu kubwa ya mapato ya ndani kufanya kazi ya ujenzi na uendelezaji wa miradi mbalimbali katika jamii kumeongeza uaminifu baina ya Serikali na wananchi pamoja na ushirikiano baina ya watumishi wa idara ya fedha na idara nyingine ni masuala yaliyochangia kufanikisha ukusanyaji wa mapato uliovuka malengo.

Kwa upande wake Afisa Mapato wa Halmashauri ya Mji wa Geita Ndg. Goodluck Nkwabi amefafanua kuwa ufuatiliaji wa karibu wa makusanyo katika vyanzo mbalimbali vya mapato na ushuru wa vibanda ambayo ni tozo mpya iliongezeka kutoka shilingi elfu 10 hadi shilingi 30,000/= kuanzia mwezi Januari 2018 sababu iliyowezesha kupandisha kwa kasi makusanyo ya mapato kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Akibainisha mikakati iliyowekwa katika mwaka mpya wa fedha 2018/2019 Ndg. Kakulima amesema kuwa Halmashauri imejipanga kuimarisha kanzu data( Data base) ya walipa kodi ili kuweza kutambua walipa kodi wa zamani na wapya, sambamba na kuanzisha madaftari ya walipa kodi katika kila mtaa na kata shughuli inayofanywa kwa ushirikiano na watendaji wa mitaa.

Ndg. Kakulima ameongeza kuwa ujenzi ulioanza hivi karibuni wa maduka ya kisasa kuzunguka soko kuu la Geita mjini ambayo yanajengwa kupitia fedha za Miradi ya jamii( CSR) kutoka Mgodi wa Dhahabu wa Geita pamoja na kuweka mazingira rafiki kwa wachenjuaji na wachomaji wa dhahabu baada ya Serikali kudhibiti uvushaji wa kaboni kutoka Mkoa wa Geita kwenda mikoa ya jirani kutaongeza mapato ya Halmashauri kwa mwaka mpya wa fedha ulioanza mwezi Julai 2018.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa