• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Mji Yabuni Mkakati Wa Uboreshaji Usafi

Posted on: July 4th, 2023

Geita Mji Yabuni Mkakati Wa Uboreshaji Usafi

Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira Halmashauri ya Mji wa Geita Ndg. Aloys Mutayuga ameeleza kuwa Halmashauri yake imeanza kutekeleza mradi wa maboresho ya ukusanyaji, uhifadhi na uchakataji wa taka kwa lengo la kuimarisha usafi wa mazingira na kuongeza mapato kupitia taka.

Kupitia mradi huu wananchi watapata furs aya kutupa aina mbalimbali za uchafu katika chombo maalum kwa aina ya taka aliyonayo, mfano chupa za maji, mabaki ya vyakula, makaratasi nk hayatachanganywa katika chombo kimoja bali kila aina ya taka itatupwa katika chombo chake kilichobainishwa kwa maandishi yanayosomeka katika masanduku hayo.

Ndg. Mutayuga amebainisha hayo hivi karibuni wakati wa zoezi la kusambaza makontena Matano ya kuhifadhia taka kwa kila kituo katika vituo kumi mjini Geita ili kutoa fursa kwa watupa taka kutenganisha taka na kurahisisha uchakataji.

“Utenganishaji wa taka utafanikisha mradi wa Halmashauri wa kuzifanyia taka urejeshaji(recycling) kwa kuzalisha mbolea kutoka taka ozo, kuzalisha mkaa kwa makaratasi na taka za plastiki ambazo zitauzwa viwandani. Pia zoezi hili litatuwezesha kutambua aina ya takataka inayozalishwa kwa wingi katika mji wa Geita kuliko takataka nyinginezo.” Aliongeza Aloys Mutayuga.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Ndugu Zahara Michuzi amesema kuwa taasisi yake imejipanga kutenga bajeti ya kutosha ili kuhakikisha mradi wa uchakataji taka unafanikiwa na kuwa endelevu kwa lengo la kuimarisha usafi wa mji na kuongeza mapato kila mwaka wa fedha.

Bahati Godwin ambaye ni mkazi wa Geita mjini ametoa pongezi za dhati kwa Halmashauri ya Mji wa Geita kwa kuwawekea vifaa vingi vya kutupia taka katika maeneo mbalimbali ya makazi yao na kuahidi kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kila mwananchi ameelewa matumizi sahihi ya vifaa hivyo.

Kulingana na takwimu zilizotolewa na Kitengo cha Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira   hadi  sasa Halmashauri ina uwezo wa kukusanya tani 2800 kati ya tani 5700 za taka zinazozalishwa kwa mwezi, saw ana ufanisi wa asilimia 49 huku lengo likiwa ni kufikia ufanisi wa asilimia 60 katika mwaka wa fedha 2023/2024.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa