• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Mji Kuanza Utekelezaji wa Mradi wa TACTIC

Posted on: October 25th, 2023

Geita Mji Kuanza Utekelezaji wa Mradi wa TACTIC

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa zaidi ya Shilingi Bilioni 22 kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa kilomita 17 za Barabara kwa kiwango lami ya zege (Asphalt Concrete) katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Mji Geita kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji Tanzania(TACTIC).

Akizungumza wakati wa mkutano wa kuanza kwa utekelezaji wa mradi wa Uboreshaji wa Mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa EPZA Bombambili Geita mjini tarehe 24/10/2023, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Cornel Magembe ametoa shukrani za dhati kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuipatia Geita Mji fedha nyingi za utekelezaji wa mradi huo utakaoleta maendeleo kwa wananchi.

Mkuu wa wilaya ya Geita ameeleza kuwa kwa niaba ya wananchi wa Mji wa Geita wameupokea mradi huo kwa moyo mkunjufu na kuwaelekeza watendaji na wenyeviti wa mitaa kuhakikisha wanafikisha taarifa sahihi za kuanza kwa mradi huu kwa wananchi katika mitaa yote inayopitiwa na Barabara hizo ili wananchi watoe ushirikiano wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

“Mkandarasi uliyepewa dhamana ya ujenzi wa Barabara katika mji wetu nawaagiza kuhakikisha anajenga Barabara hizo katika ubora wa hali ya juu na kukamilika ndani ya miezi 15 kama walivyokubaliana kwenye mkataba ili mradi huo uweze kuwanufaisha wananchi na Wilaya nzima kwa ujumla”. Aliongeza Mhe. Cornel Magembe.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Bw. Lee Joshua amesema kuwa baada ya mradi kukamilika utabadilisha muonekano wa mji wa Geita, kutoa ajira kwa wananchi wa Mji wa Geita kupitia shughuli mbalimbali zinazohusiana na utekelezaji wa mradi huo pamoja na kupunguza msongamano wa magari na vyombo vingine vya usafiri.

Mwakilishi wa Mkandarasi M/s Sichuan Road & Bridge (Group) Corporation Limited wa Dar es Salaam ambaye amesaini mkataba wa utekelezaji wa mradi huo utakaoanza mapema mwezi Novemba 2023 Ndg. SIBO ameahidi kutoa ushirikiano kwa timu ya wataalam wa Halmashauri na Wakala wa Barabara vijijini na mjini(TARURA), Viongozi kuanzia ngazi ya mtaa, kufuata mkataba unavyoeleza. Kuajiri wafanyakazi kulingana na sheria za Nchi na kukamilisha mradi ndani ya muda uliopangwa na katika kiwango cha hali ya juu.

Mradi wa Ujenzi wa Kilomita 17 za Barabara Geita mjini utakuwa chini ya Mkandarasi Mshauri M/s Luptan Consults Limited akishirikiana na SAFI Consultants Limited wa Dar es Salaam ambapo Barabara zitakazojengwa ni Barabara ya Mkolani- Mwatulole km 5.9, Nyankumbu- Kivukoni km 3.9, Ngunzombili-Samandito-Emma-Mama Kengele km 3.3, Mwatulole-Mshinde- Twiga- Geita Gold Refinery km 3.9







Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa