• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Mji Kinara Utoaji Mikopo kwa Vikundi

Posted on: July 12th, 2019

Geita Mji Kinara Utoaji Mikopo kwa Vikundi

Halmashauri ya Mji wa Geita imekuwa Halmashauri ya kwanza katika Mkoa wa Geita kwa kutoa kiasi kikubwa cha fedha kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu, mikopo isiyo na riba ambayo ni asilimia 10% ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mfuko wa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu wakati wa hafla fupi ya utoaji Hundi kwa vikundi 40 iliyofanyika katika Ukumbi wa Gedeco Halmashauri ya Mji Geita Tarehe 12/7/2019 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Mji Geita Ndg. Majagi Maiga amesema kuwa Halmashauri ya Mji Geita imefanikiwa kutoa jumla ya Shilingi 706,000,000/=( Milioni Mia saba na sita) kwa vikundi 149 katika mwaka wa fedha 2018/2019.

Ndg. Majagi amefafanua kuwa kiasi cha Shilingi 419,000,000/= zimekopeshwa kwa vikundi 93 vya wanawake, Shilingi 262,000,000/= zimekopeshwa kwa vikundi 51 vya vijana na vikundi 5 vya watu wenye ulemavu vimekopeshwa Shilingi 25,000,000/=. Pia vikundi vinaendelea kurejesha ambapo hadi mwaka wa fedha unaisha jumla ya Shilingi 52,235,000/= zimerejeshwa kutoka kwa baadhi ya vikundi vilivyokopeshwa.

Akiongea wakati wa kukabidhi hundi kwa vikundi 40 vya awamu ya mwisho kwa mwaka wa fedha 2018/2019. Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amewaasa wanavikundi waliopatiwa mkopo kutambua kuwa fedha wanazokopeshwa ni maalum kwa ajili ya kuwasaidia kutekeleza mipango waliyopanga kwa ajili ya kujipatia maendeleo na si fedha ya kufanyia starehe au shughuli binafsi zisizo na manufaa.

Mhandisi Robert Gabriel ametumia fursa hiyo kuwaagiza wataalam wa Idara ya Maendeleo ya Jamii kutembelea vikundi na kufanya tathmini ili kubaini vikundi hai vyenye malengo na vinafanya vizuri kwenye shughuli zao. Kadhalika vikundi vipatiwe uwezo ili vipate ushauri wa namna ya kuendesha biashara zao ili kuwawezesha wanakikundi kutimiza malengo yao.

Bi. Anneth Jummanne mwanakikundi wa Yes we can social group kutoka mtaa wa Kagera kata ya Kalangalala ametoa shukrani kwa kuwatambua na kuwapa mikopo isiyo na riba. Pia wameahidi kuzitendea haki fedha walizopewa kwa kuzitumia katika shughuli zao za ujasiriamali na kuzirejesha kwa wakati.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • DC KOMBA AWAKARIBISHA NACHINGWEA KUJIFUNZA UCHIMBAJI GEITA, ATOA USHAURI WA NAMNA NZURI YA USIMAMIZI WA MIGODI

    June 26, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa