• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Kunufaika Na TASAF Awamu ya Nne

Posted on: November 1st, 2021

Geita Kunufaika Na TASAF Awamu ya Nne

Kiasi cha Dola milioni 50 zimetengwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya kutoa ajira za muda kwa walengwa wa mpango wa kupunguza umaskini na uendelezaji wa miundombinu ya kutolea huduma za jamii kama elimu, afya na maji katika mikoa mitano ambayo ni Geita, Mwanza, Simiyu, Arusha na Njombe kuanzia mwaka 2021 hadi 2025.

Akizungumza wakati wa kikao kazi cha kujenga uelewa wa Pamoja juu ya mradi wa kupunguza umaskini awamu ya nne na kubadilishana uzoefu kutoka kwa waratibu wa Mkoa wa Geita katika ukumbi wa Uwekezaji kiuchumi Bombambili Geita mjini hivi karibuni, Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Ladslaus Mwamanga ameshauri kuwa kusiwe na mrundikano wa utoaji wa huduma katika eneo moja bali fursa zitawanywe kwenye maeneo yenye uhitaji yatakayobainishwa na wanajamii wa maeneo husika.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Staki Senyamule ameishukuru Serikali chini ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zenye lengo la kuongeza fursa za kujiongezea kipato na kuboresha huduma za kiuchumi na kijamii kwa kaya za walengwa pia kulinda maslahi ya familia zao na jamii kwa ujumla.

Mhe. Senyamule ameongeza kuwa matarajio ya viongozi ni kuwa utekelezaji wa miradi hii utatoa njia mbadala za ajira kwa walengwa na kuwawezesha kushiriki katika kazi za jamii ili kupata kipato cha ziada kwa matumizi ya kaya ambacho kitawawezesha kuboresha miundombinu ya kijamii, kuwajengea ujuzi na stadi za Maisha walengwa watakaoshiriki katika kazi na kugharamia mahitaji mbalimbali ya msingi kwenye kaya zao.

Mkuu wa Mkoa wa Geita amewaagiza wasimamizi wote wa kisekta kuhakikisha wanasimamia na kufuatilia kwa karibu kila hatua ya utekelezaji wa mradi na kuepuka ubadhirifu au uhujumu wa fedha na vifaa, tabia hiyo haitavumilika bali hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya msimamizi au kiongozi yeyote atakayebainika.

“Kukamilika kwa miradi itakayopangwa kwa viwango vilivyowekwa na kutoa huduma kwa walengwa kwa wakati kitakuwa ni kipimo tosha cha ufanisi wenu katika kutekeleza majukumu  ya kila siku kwa ajili ya maendeleo endelevu wanayotamani kuyafikia wananchi wa Mkoa wa Geita. Hivyo wataalamu mnatakiwa kutekeleza miradi yote kwa weledi na kuzingatia miongozo.” Aliongeza Mhe. Senyamule.

Diwani wa Kata ya Kalangalala Mhe. Prudence Temba ambaye alimuwakilisha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuukumbuka Mkoa wa Geita katika mradi huo na kuwashauri viongozi wa TASAF kuwapatia elimu hiyo Madiwani wote ili wasaidie katika usimamizi wa miradi ambayo itatekelezwa katika maeneo yao ya utawala kwa uadilifu na uaminifu wa hali ya juu.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa