• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Bila UKIMWI Inawezekana

Posted on: December 4th, 2017

Geita Bila UKIMWI Inawezekana

Wadau wa maendeleo katika mji wa Geita wamebaini baadhi ya changamoto ambazo zikitatuliwa zitasaidia kupunguza maambukizi ya Virusi vya UKIMWI katika mji wa Geita. Changamoto hizo zimebainishwa  wakati wa kongamano la kujadili hali halisi ya maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI na kuweka mikakati ya kupunguza maambukizi hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji hivi karibuni.

Askofu Stephano Sabuda ambaye ni Mwenyekiti msaidizi wa jumuia ya Interfaith amesema kuwa elimu dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI inatakiwa ifikishwe katika jamii kwa sehemu kubwa.  Amefafanua kuwa wananchi waishio maeneo ya vijijini hawana elimu ya kutosha juu ya ugonjwa wa UKIMWI na athari zake katika jamii, hivyo watumishi wa Mungu, watu waishio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI pamoja na wataalamu wa masuala ya UKIMWI kutoka Serikalini na Taasisi binafsi washirikishwe katika utoaji wa elimu hiyo.

Mwenyekiti wa watu waishio na Virusi vya UKIMWI Geita mjini amesema kuwa sehemu kubwa ya watu wanaoishi na maambukizi ya ugonjwa huo bado wamejificha, hawataki kujitangaza hadharani au kuwashirikisha ndugu zao wa karibu. Amesema kuwa kitendo cha kujificha ni kujinyanyapaa wenyewe binafsi na kuendelea kueneza maambukizi katika jamii wanamoishi. Hivyo ametoa wito kwa watu hao kutoficha hali zao za kiafya.

Kwa upande wa mwakilishi wa wazazi amesema kuwa wazazi wanatakiwa wabadilike katika malezi kwani kwa sasa wamesahau wajibu wao kama walezi wa watoto kwa kujishughulisha zaidi na majukumu ya kiuchumi, pia kuvaa mavazi yasiyokuwa na maadili kama wazazi na kuwanunulia watoto mavazi yasiyoendana na maadili ya kitanzania.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mh. Leonard K. Bugomola amewaahidi wanachama wa KONGA kuwa Halmashauri itawalipia kodi ya pango la ofisi na kuagiza idara ya Maendeleo ya Jamii iwapatie mkopo umoja wa watu waishio na Virusi vya UKIMWI ili waweze kujikwamua kiuchumi. Pia amewaagiza walimu wakuu wa shule zote katika Halmashauri ya Mji wa Geita kuhakikisha sherehe zote mashuleni zinafanyika mchana na kumalizika saa 12 jioni.

Mratibu wa UKIMWI wa Halmashauri ya Mji Geita Bi. Mariam John amesema kuwa kitengo chake kinaendelea na zoezi la uundaji wa vikundi vya watu waishio na Virusi vya UKIMWI na kuendesha mafunzo ya ujasiriamali ili kujiingizia kipato na kujikwamua kiuchumi, pia kuwakopesha mikopo yenye riba nafuu ili waweze kuanzisha biashara na miradi mbalimbali.

Takwimu zinaonyesha kuwa kila mwaka maambukizi mapya 54,000 hadi 56,000 hujitokeza katika nchi ya Tanzania. Kauli mbiu ya maadhimisho ya UKIMWI kwa mwaka 2017 ni “Changia mfuko wa udhibiti wa UKIMWI nchini uokoe maisha, Tanzania Bila UKIMWI inawezekana.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa