• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Fugeni Nyuki Kibiashara - Kanyasu

Posted on: August 14th, 2019

Fugeni Nyuki Kibiashara- Kanyasu

Wanavikundi wanaojishughulisha na ufugaji nyuki katika Wilaya ya Geita wameshauriwa kufanya shughuli hiyo kwa malengo ili kufanya ufugaji wa nyuki kuwa wa kibiashara zaidi.

Ushauri huo umetolewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Costantine Kanyasu alipokuwa akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Geita ambao wameunda vikundi vya ufugaji nyuki hivi karibuni katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ambapo pia aligawa mizinga ya nyuki kwa vikundi hivyo.

Mheshimiwa Kanyasu ameongeza kuwa Wizara yake imeamua kufanya zao la nyuki kuwa moja ya zao la kibiashara katika mikoa minane ikiwemo Geita hivyo wakazi wa Geita wanatakiwa watumie fursa hiyo kwa kutofuga nyuki kwa mazoea kama zamani.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii amesema kuwa Serikali itatoa mashine za kisasa kwa ajili ya kuchakata asali katika mikoa yote ya ukanda wa asali hivyo wafugaji hao wanatakiwa wasimamie na kutunza vizuri maeneo ambapo mizinga itawekwa kwa kulinda vyanzo vya maji kwani hakuna maisha ya nyuki bila maji. Pia aliwataka wafugaji kulinda misitu isichomwe moto.

Mheshimiwa C. Kanyasu alitumia fursa hiyo kuwaagiza wataalam wa Wakala wa huduma za  Misitu Tanzania kuhakikisha wanakuwa karibu na vikundi vilivyopata mafunzo ya ufugaji nyuki ili kuwasaidia katika shughuli zao za ufugaji na kutatua changamoto zinazowakabili.

Akizungumzia changamoto zinazoikabili sekta ya ufugaji Meneja misitu wa Wilaya ya Geita Ndg. Fredy Ndandika amesema kuwa uvamizi na uharibifu wa misitu kwa shughuli za kilimo, ukataji miti, moto kichaa na malisho ya mifugo pamoja na ukosefu wa soko la kudumu la mazao ya nyuki ambayo ni asali na nta ni kati ya changamoto ambazo huathiri maendeleo ya ufugaji nyuki.

Katika ziara yake ya kikazi Wilayani Geita Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Costantine Kanyasu amegawa mizinga ipatayo 200 kwa vikundi 10 kutoka Halmashauri mbili za Wilaya ya Geita ambavyo vilipata fursa ya kuwezeshwa mafunzo ya namna ya ufugaji wa kisasa wa nyuki, mafunzo yaliyotolewa na Wakala wa huduma za Misitu Wilaya ya Geita.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa