• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Fanyeni Kazi Kwa Maadili na Ubunifu - RC Geita

Posted on: May 3rd, 2023

Fanyeni Kazi Kwa Maadili na Ubunifu- RC Geita

Wafanyakazi wa sekta binafsi, mashirika, Taasisi na watumishi wote wa umma katika mkoa wa Geita wameaswa kuhakikisha wanatimiza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za kazi katika shughuli zao sambamba na kuongeza ubunifu katika majukumu yao ya kila siku.

Ujumbe huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela alipokuwa akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya wafanyakazi duniani tarehe 01/5/2023 yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya CCM Kalangalala Geita mjini.

Mhe. Shigela ameongeza kuwa kila mfanyakazi katika eneo lake la kazi anao wajibu wa kufanya kazi kwa bidii ili kuongeza ufanisi wa kazi na endapo kila mmoja atatimiza wajibu wake kikamilifu basi ataboresha kiwango cha kipato kuanzia ngazi ya familia hadi Taifa kwa ujumla.

Mkuu wa Mkoa wa Geita amewasisitiza waajiri kutenga bajeti ya kuwapeleka watumishi wao kwenye mafunzo mbalimbali kwa lengo la kuboresha maslahi na mazingira rafiki kwa mfanyakazi ili kuongeza tija na ufanisi kwenye taasisi na kukabiliana na changamoto mpya za maendeleo katika utendaji kazi.

Mhe. Shigela amekemea tabia ya baadhi ya waajiri ambao wanahamisha watumishi bila mpangilio wala kuwa na bajeti hiyo, amesema kuwa kuna watumishi wakifanya makosa wanapewa uhamisho kwenda vituo vingine vya kazi kama sehemu ya adhabu,suala hili sio sahihi na lisitishwe mapema iwezekanavyo kwani kumuhamisha mtumishi pasipokuwa na bajeti ni kuiongezea Serikali mzigo. Mtumishi akikosea hatua za kinidhamu zichukuliwe katika eneo lake analofanyia kazi na sio kumuhamisha.

 Akitoa salamu za Mei mosi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Ndugu Zahara Michuzi ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wafanyakazi kupitia fedha za miradi mbalimbali kama madarasa na nyumba za watumishi na kuahidi kuendelea kutenga bajeti ya kuwapeleka watumishi wao kila mwaka wa fedha kwenye mafunzo ya muda mfupi na mrefu ili kuendelea kuwa na watumishi mahiri katika fani mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini (TUCTA) Ndg. Obed Mwakapango ameiomba Serikali kuingilia kati katika kutafuta suluhisho la changamoto mbalimbali ambazo bado zinawakabili  wafanyakazi katika maeneo yao ya kazi ikiwemo malimbikizo ya mishahara, taasisi binafsi kutozingatia viwango vipya vya mishahara, na baadhi ya waajiri kutopeleka michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.

Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani mwaka 2023 yameadhimishwa kitaifa katika mkoa wa Morogoro na kuhudhuriwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yakiwa yamebeba kauli mbiu isemayo ‘’Mishahara Bora na Ajira za staha ni Nguzo kwa Maendeleo ya Wafanyakazi, Wakati ni sasa’’.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KOZI YA AWALI YA JESHI LA AKIBA WAPATIWA ELIMU YA HABARI

    July 04, 2025
  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa