• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Nyuki na Misitu
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Familia Zahimizwa Kutatua Migogoro Kwa Upendo

Posted on: December 14th, 2022

Familia Zahimizwa Kutatua Migogoro Kwa Upendo

Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Mji Geita Bi. Margareth Macha ametoa wito kwa familia kuhakikisha wanatatua migogoro yao kwa amani na upendo ili kuepukana na tatizo la kusambaratika kwa familia kunakochangia ongezeko la vitendo vya ukatili katika jamii hususani kwa Watoto.

Bi. Macha ameyasema hayo hivi karibuni alipomuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Geita wakati wa kongamano la kuhitimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambalo limefanyika katika ukumbi wa eneo maalum la uwekezaji kiuchumi Bombambili mjini Geita.

Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji ameongeza kuwa vitendo vya ukatili ambavyo vimeendelea kushamiri katika jamii kwa kiasi kikubwa vinachangiwa na vurugu za kifamilia, ambapo baada ya wazazi kugombana na kuachana Watoto wengi wanabaki wanajilea wenyewe hali inayopelekea baadhi ya watu wasio na utu kuwafanyia matendo ya kikatili.

“Asilimia kubwa ya wazazi katika jamii za wachimbaji madini wameacha majukumu ya malezi kwa Watoto baada ya wao Kwenda kutafuta riziki katika maeneo mbalimbali ya uchimbaji dhahabu. Wazazi mnatakiwa kubadilika na kutimiza wajibu wenu wa malezi ya Watoto na kila mwananchi awe balozi wa mwingine katika kutoa ushirikiano kwa kutoa Ushahidi juu ya matukio ya ukatili wa kijinsia yanapofanyika katika jamii”.

Kwa Upande wake Afisa Maendeleo Mkoa wa Geita Ndg. Elikana Haruni amewaasa wananchi wilayani Geita kuachana kabisa na mila pamoja na desturi ambazo kwa namna moja au nyingine zinaendelea kukandamiza Watoto wa kike na kusababisha ukatili wa kijinsia.

Mtaalam kutoka taasisi ya Marafiki wa Elimu Geita Bw. Ayoub Bwanamadi amewataka wananchi kuripoti matukio yote ya kikatili yanayotokea katika jamii yao na kutomaliza kesi za ukatili kienyeji au kindugu hususan kwa wanawake ambao wanaogopa kuripoti juu ya ukatili unaofanywa na waume zao majumbani kwa hofu ya kuachwa na kuchukiwa na familia za upande wa mume.

Ndugu Bwanamadi ameeleza kuwa jamii inapaswa kutambua kuwa sheria zipo kwa ajili ya utekelezaji wa haki, endapo wananchi wataendelea kuficha matukio ya ukatili wa kijinsia yanayoendelea kwenye jamii yao kwa kuhofia sheria kuchukua mkondo wake basi matukio hayo hayatatokomezwa asiliani.

Maadhimisho ya kuhitimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia katika jamii yaliongozwa na kauli mbiu isemayo “Kila uhai una thamani,Tokomeza mauaji na Ukatili dhidi ya wanawake na Watoto”. Ambapo yalienda sambamba na hitimisho la wiki ya msaada wa kisheria katika Halmashauri ya Mji Geita iliyobeba kauli mbiu isemayo “Ukatili na Udhalilishaji wa kijinsia ni kikwazo kwa maendeleo ya Taifa, wananchi wote Tusimame kuzuia”.



Matangazo

  • TANGAZO LA URASIMISHAJI WA MAKAZI YASIYOPANGWA January 16, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI July 22, 2022
  • TANGAZO LA KAZI ZA MACHINJIO August 16, 2022
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA GEITA MJI December 02, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Kamati Ya Siasa Wilaya Ya Geita Yaridhishwa na Miradi Geita Mji

    January 26, 2023
  • Walimu 668 Geita Mji Wanufaika na Vishikwambi

    January 18, 2023
  • Wanufaika Washauriwa Kuanzisha Viwanda Vidogo

    December 27, 2022
  • Timu Ya Halmashauri Yapata Udhamini Kutoka GGM

    December 20, 2022
  • Zaidi

Video

Machinjio ya Kisasa Mpomvu Yaanza kazi
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa