• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Familia Zahimizwa Kutatua Migogoro Kwa Upendo

Posted on: December 14th, 2022

Familia Zahimizwa Kutatua Migogoro Kwa Upendo

Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Mji Geita Bi. Margareth Macha ametoa wito kwa familia kuhakikisha wanatatua migogoro yao kwa amani na upendo ili kuepukana na tatizo la kusambaratika kwa familia kunakochangia ongezeko la vitendo vya ukatili katika jamii hususani kwa Watoto.

Bi. Macha ameyasema hayo hivi karibuni alipomuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Geita wakati wa kongamano la kuhitimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambalo limefanyika katika ukumbi wa eneo maalum la uwekezaji kiuchumi Bombambili mjini Geita.

Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji ameongeza kuwa vitendo vya ukatili ambavyo vimeendelea kushamiri katika jamii kwa kiasi kikubwa vinachangiwa na vurugu za kifamilia, ambapo baada ya wazazi kugombana na kuachana Watoto wengi wanabaki wanajilea wenyewe hali inayopelekea baadhi ya watu wasio na utu kuwafanyia matendo ya kikatili.

“Asilimia kubwa ya wazazi katika jamii za wachimbaji madini wameacha majukumu ya malezi kwa Watoto baada ya wao Kwenda kutafuta riziki katika maeneo mbalimbali ya uchimbaji dhahabu. Wazazi mnatakiwa kubadilika na kutimiza wajibu wenu wa malezi ya Watoto na kila mwananchi awe balozi wa mwingine katika kutoa ushirikiano kwa kutoa Ushahidi juu ya matukio ya ukatili wa kijinsia yanapofanyika katika jamii”.

Kwa Upande wake Afisa Maendeleo Mkoa wa Geita Ndg. Elikana Haruni amewaasa wananchi wilayani Geita kuachana kabisa na mila pamoja na desturi ambazo kwa namna moja au nyingine zinaendelea kukandamiza Watoto wa kike na kusababisha ukatili wa kijinsia.

Mtaalam kutoka taasisi ya Marafiki wa Elimu Geita Bw. Ayoub Bwanamadi amewataka wananchi kuripoti matukio yote ya kikatili yanayotokea katika jamii yao na kutomaliza kesi za ukatili kienyeji au kindugu hususan kwa wanawake ambao wanaogopa kuripoti juu ya ukatili unaofanywa na waume zao majumbani kwa hofu ya kuachwa na kuchukiwa na familia za upande wa mume.

Ndugu Bwanamadi ameeleza kuwa jamii inapaswa kutambua kuwa sheria zipo kwa ajili ya utekelezaji wa haki, endapo wananchi wataendelea kuficha matukio ya ukatili wa kijinsia yanayoendelea kwenye jamii yao kwa kuhofia sheria kuchukua mkondo wake basi matukio hayo hayatatokomezwa asiliani.

Maadhimisho ya kuhitimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia katika jamii yaliongozwa na kauli mbiu isemayo “Kila uhai una thamani,Tokomeza mauaji na Ukatili dhidi ya wanawake na Watoto”. Ambapo yalienda sambamba na hitimisho la wiki ya msaada wa kisheria katika Halmashauri ya Mji Geita iliyobeba kauli mbiu isemayo “Ukatili na Udhalilishaji wa kijinsia ni kikwazo kwa maendeleo ya Taifa, wananchi wote Tusimame kuzuia”.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa