• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Elimu ya MWEMKWA Mkombozi kwa Watoto

Posted on: May 25th, 2018

Mfumo wa MWEMKWA Mkombozi kwa Watoto

Mfumo wa elimu ya msingi usio rasmi( MWEMKWA) unaowawezesha wanafunzi kuanzia umri wa miaka 9 hadi 13 ambao hawakupata nafasi ya kuanza elimu ya Msingi wakiwa na umri wa miaka 7 kwa sababu mbalimbali umebainika kuwanufaisha watoto wanaoandikishwa katika  darasa hilo.

Akizungumza hivi karibuni wakati wa maadhimisho ya juma la Elimu katika Halmashauri ya Mji wa Geita Mwalimu Bahati Gabriel kutoka shule ya Msingi Mseto, ambaye ni mwalimu wa darasa la MWEMKWA amesema kuwa wanafunzi wake wanafundishwa kusoma,kuhesabu na kuandika na wakishaelewa wanaingizwa darasa la nne katika mfumo rasmi kwa ajili ya kufanya mtihani wa Taifa, wakishafaulu wanaendelea na darasa la tano pamoja na wanafunzi wengine.

Katika maadhimisho ya juma la Elimu kwa mwaka huu, wataalam wa Idara ya elimu walitembelea shule mbalimbali za msingi  ili kukagua shughuli za ufundishaji wanafunzi zinazofanyika kila siku na changamoto wanazokabiliana nazo walimu na wanafunzi katika utendaji kazi wao.

Mwanafunzi wa darasa la MWEMKWA, Marko John amesema kuwa alichelewa kuanza shule baada ya wazazi wake kutengana na kuachwa kijijini na bibi yake ambaye hakuwa na uwezo wa kumnunulia mahitaji ya muhimu kwa ajili ya kuanza shule. Baada ya miaka kadhaa mjomba wake alimchukua na kumleta Geita mjini ambapo alimwandikisha shule. Marko ana malengo ya kuwa Daktari ili aisaidie jamii ambayo haina uwezo.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mseto Bi. Grace Mutabuzi amefafanua kuwa watoto wengi wanajilea wenyewe na wengi wao wanafika kujiandikisha shule wao binafsi, ambapo walimu huchukua jukumu la kuwatembelea wazazi/ walezi wa wanafunzi majumbani na kuwaelimisha juu ya umuhimu wa elimu. Ameeleza kuwa sababu kubwa ya watoto kuchelewa kuanza shule ni kitendo cha watoto hao kushirikishwa katika shughuli mbalimbali za kiuchumi kama kilimo, upondaji mawe, uchimbaji mdogo na biashara ndogondogo.

Bi. Grace Mutabuzi amefafanua kuwa changamoto wanazokabiliana nazo katika ufundishaji wa darasa la MWEMKWA ni utoro wa rejereja ambapo baadhi ya wanafunzi hawafiki shule kwa wiki mbili hadi tatu kwa sababu ya kwenda kujitafutia riziki na mahitaji mbalimbali. Pia hakuna ushirikiano baina ya wazazi/walezi na walimu.

Kadhalika Mwalimu Mkuu huyo ameongeza changamoto nyingine kuwa ni baadhi ya wanafunzi huacha shule baada ya kujua kusoma na kuandika. Pia wengine kutofanya mtihani baada ya kusajiliwa, akitolea mfano wa wanafunzi  wanne kati ya sita waliokuwa wameandikishwa kwa ajili ya mtihani wa Taifa wa darasa la nne Mwaka 2017  kuacha shule kabla hawajafanya mtihani huo.

Mwalimu Grace Mutabuzi na Afisa Elimu ya Msingi katika Halmashauri ya Mji wa Geita Bw. Yesse Kanyuma wana matumaini ya kuwavusha wanafunzi wa darasa la MWEMKWA ambao wataonyesha bidii ya kufikia ndoto zao, kwani kuna wanafunzi ambao kwa sasa ni walimu, wako vyuo vikuu, wanajishughulisha na biashara zao ambao ni matunda yaliyopatikana kupitia elimu ya MWEMKWA.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa