• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Elimu ya Lishe Ibadilishe Mazoea Katika Jamii

Posted on: June 6th, 2024

Elimu ya Lishe Ibadilishe Mazoea katika Jamii- DAS Geita

Kina mama walioko katika Halmashauri ya Mji Geita wameshauriwa kutumia fursa ya elimu ya lishe wanayopatiwa na wataalam wa Kitengo cha lishe ili kubadilisha mazoea ya uandaaji wa uji wa Watoto ambao hauzingatii lishe bora.

Ushauri huo umetolewa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Geita Ndugu. Lucy Beda alipokuwa akiongea na wananchi waliohudhuria uzinduzi wa Kampeni ya utoaji matone kwa Watoto wenye umri chini ya miaka mitano ambayo imefanyika tarehe 05/06/2024 katika kituo cha afya Nyankumbu.

Katibu Tawala Wilaya ya Geita ameeleza kuwa wataalam wa Kitengo cha lishe katika majukumu yao ya kila siku wameendelea kutoa elimu ya uandaaji wa uji wa Watoto kwa kuzingatia makundi sita ya vyakula ambayo ni nafaka mizizi na ndizi za kupika ,mbogamboga,matunda, vyakula vya asili ya nyama, kunde na mafuta na elimu ya unyonyeshaji kwa Watoto wachanga

Hivyo wazazi na walezi waliokuwa na mazoea ya kuweka kundi la wanga pekee kwenye uji wa Watoto wabadilike na kufuata kanuni za uandaaji wa lishe inayofaa kwa makuzi bora ya Watoto na kuepukana na tatizo la udumavu na utapiamlo mkali kwa Watoto.

Kaimu Afisa Tarafa wa Geita mjini Ndugu Cosmas Bayaga ametoa rai kwa wataalam wa kitengo cha lishe kutembelea shule mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu kuhusu maandalizi ya uji wenye mchanganyiko wa makundi yote ya chakula na kuachana na tabia ya kupika uji kwa mazoea.

Kwa upande wa Mganga mkuu wa Halmashauri ya Mji Geita Daktari Sunday Mwakyusa amesema kuwa changamoto kama uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora kwa kuzingatia makundi sita ya vyakula, matone ya Vitamin A na dawa za minyoo pamoja na mapokeo hasi ya baadhi ya wazazi/walezi juu ya dawa za chanjo hupelekea kutokea kwa magonjwa ya Watoto kama vile minyoo, surau na uoni hafifu.

Dkt. Mwakyusa amesema kuwa Halmashauri ya Mji Geita imejipanga kufikia Watoto 55,710 wenye umri wa miezi 6 hadi 59 ambao watafikiwa kwa njia za kliniki za mkoba, kliniki ya baba, mama na mtoto vituoni na kwenye vituo na kwenye vituo vyote vya kutolea huduma huduma za afya sambamba na kufanya upimaji wa hali ya lishe kwa Watoto wenye umri chini ya miaka mitano.





Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa