• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Bilioni 9.8 Kutekeleza Miradi Geita Mji Kupitia CSR

Posted on: March 22nd, 2023

Bilioni 9.8 Kutekeleza Miradi Geita Mji Kupitia CSR

Halmashauri ya Mji Geita na Kampuni ya Mgodi wa Dhahabu Geita (GGML) wamesaini mkataba wa makubaliano ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ambayo itatekelezwa kupitia fedha za uwajibikaji wa kampuni kwa jamii (CSR) kwa kipindi cha miaka miwili 2022 na 2023, ambapo Halmashauri ya Mji wa Geita itatumia Shilingi Bilioni 9.8 katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Akizungumza katika hafla fupi ya utiaji Saini wa Mkataba wa makubaliano hayo baina ya Halmashauri ya Mji Geita na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML) iliyofanyika tarehe 21/3/2023 katika ukumbi wa Mchauru Village Geita mjini, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela ametoa shukrani za dhati kwa Mgodi wa GGM kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kuwahimiza wawekezaji wengine ndani ya mkoa wa Geita kuiga mfano wa kampuni ya GGM katika kuhudumia jamii inayowazunguka.

Mkuu wa Mkoa wa Geita amewaagiza watekelezaji wa miradi hiyo kuhakikisha mchakato wa kutafuta wakandarasi wa ujenzi wa miradi hiyo uanze mapema ili ifikapo mwezi wa tano mwaka 2023 ujenzi wa miradi hiyo uwe umeanza. Pia fedha zilizoidhinishwa katika hati ya makubaliano zitumike katika miradi iliyoainishwa kwenye mpango wa makubaliano kwa wakati uliopangwa na katika ubora wa hali ya juu ili iweze kuleta tija kwa wananchi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Geita Mheshimiwa Costantine Morandi amesema 1/3 ya mapato ya ndani yanayokusanywa na Halmashauri yake yanatoka kwenye Mgodi wa GGM na yameiwezesha kujenga zahanati Zaidi ya 20 pamoja na utekelezaji wa miradi mingine ya michezo,barabara, elimu na pia vijana kutoka kwenye mitaa inayozunguka mgodi wananufaika na ajira kila mwaka katika mgodi huo.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Anglo Gold Ashanti Bw. Simon Shayo amesema kuwa Mgodi wa GGM unatambua thamani ya jamii inayowazunguka hivyo wanajitahidi kuhakikisha wananchi wanaishi vizuri  kupitia manufaa ya miradi ya elimu, afya, maji, kilimo, miundombinu ya barabara Pamoja na miradi ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Baadhi ya Miradi itakayotekelezwa katika mkataba wa Makubaliano ya utekelezaji wa miradi ya CSR kwa miaka miwili 2022 na 2023 ni Pamoja na ukamilishaji wa ujenzi wa uwanja wa michezo Geita mjini, ujenzi wa maduka kuzunguka Soko kuu la Dhahabu kwa awamu ya tatu, ujenzi wa daraja litakalounganisha mtaa wa Nyakabale na Kijiji cha Bugulula, Ujenzi wa Uzio katika kituo cha Afya Kasamwa na ukamilishaji wa Zahanati zilizojengwa kwa fedha za CSR miaka iliyopita ili zianze kutoa huduma kwa wananchi.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI KAZI YA MKATABA May 23, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI July 22, 2022
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA GEITA MJI December 02, 2022
  • KUSUDIO LA KUNYANG'ANYWA VIWANJA December 06, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Mbolea Kuanza Kusambazwa na Vyama Vya Ushirika

    June 09, 2023
  • Ujenzi Wa Miundombinu Ya BOOST Waanza Kwa Kishindo

    May 19, 2023
  • Fanyeni Kazi Kwa Maadili na Ubunifu - RC Geita

    May 03, 2023
  • Jamii Yashauriwa Kuwapeleka Watoto Kwenye Chanjo

    April 25, 2023
  • Zaidi

Video

MIAKA MIWILI YA MAMA SAMIA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa