Hafla ya utiaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa Kituo cha Mabasi imefanyika leo tarehe 06 Juni, 2025 katika Ukumbi wa EPZA uliopo Bombambili katika Halmashauri ya Manispaa ya Geita Mkoani Geita. Mgeni rasmi katika hafla hii alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba.
Mhe. Komba akizungumza mara baada ya kushuhudia utiaji Saini wa Mkataba huo, amemtaka mkandarasi anaetekeleza mradi huo kuhakikisha anazingatia muda wa mkataba kwa kuwa kituo kinachotumika kwa sasa hakikidhi matarajio.
“Na tumeanza safari pamoja ya kuhakikisha mkandarasi anatimiza malengo ambayo ya Mkataba, mradi huu uanze kwa wakati na ukamilike kwa wakati” Amesema Mhe. Komba
Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Mhe. Costantine Kanyasu amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa wa stendi hii ya mbasi.
Naye Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita Costantine Morandi amewashukuru wananchi kwa kuendelea kuwa wavulivu kwa kipindi kirefu wakisubiria stendi hii mpya na ya kisasa.
Wakati huo huo Mkurugenzi wa Manispaa ya Geita, Ndg. Yefred Myenzi akiwa katika hafla hiyo amesema ujenzi huo utagharimu zaidi ya Bilioni 19 ili kuondoa adha waliyokuwa wakiipata wananchi na watumiaji wote kwa ujumla katika kituo cha sasa hususani kipindi cha mvua.
“Tumefurahi kwa sababu sasa serikali imetoa pesa Bilioni 19.1 kwa ajili ya ujenzi mpya ya kisasa ambayo kama ambavyo tulivyoshuhudia mkandarasi amesaini na tumeahidiwa kwamba tarehe 15 tayari atakuwa kazini kwa ajili ya kuendelea na taratibu” amesema Myenzi
Mkataba huo umesainiwa baina ya Halmashauri ya Manispaa ya Geita na Mkandarasi M/s SIHOTECH Engineering Company Ltd. na AMJ Global Multi Contractors Company Ltd na Gharama ya Mkataba huo ni TZS 19,171,601,509.00 ambapo Muda wa utekelezaji wake ni Miezi 15 kuanzia tarehe 15 Juni, 2025 hadi tarehe 14 Septemba, 2026 na utekelezaji huu unafanyika kupitia mradi wa uboreshaji Miji Tanzania (TACTIC).
Stendi hiyo mpya itajengwa katika kiwanja namba 01, kitalu "G" chenye ukubwa wa mita za mraba 109,450 sawa na hekta 10.9 kilichopo Mtaa wa Magogo, Kata ya Bombambili. Eneo hili limetengwa mahsusi kwa matumizi ya stendi ya mabasi na linamilikiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Geita.
TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
Instagram
Geita Tanzania
Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita
Namba ya Simu: 0282520437
Mobile:
Barua pepe: td@geitatc.go.tz
Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa