• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 68.3

Posted on: January 30th, 2025

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita Mhe. Costantine Morandi Mtani Leo tarehe 30 Januari, 2025 ameongoza Mkutano wa Baraza la Madiwani, na Baraza hilo limeridhia kupitisha rasimu ya bajeti ya Shilingi Bilioni 68,393,812,906.00 kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Bajeti hii ina ongezeko la 13.2% zaidi ya ile ya mwaka wa fedha 2024/2025 Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Halmshauri wa EPZ uliopo katika Viwanja vya Maonesho.


Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita Mhe. Costantine Morandi Mtani

Kati ya bajeti hiyo shilingi bilioni 47,547,078,004.00 sawa na 69.6% ni ruzuku kutoka Serikali Kuu na Shilingi bilioni 20,846,734,902.00 sawa na 30.4% zitatokana na mapato ya ndani ambayo ni ongezeko la asilimia 4.2 kutoka bajeti ya mwaka 2024/2025 kwa Shilingi bilioni 19,965,455,000.00

Akizungumza katika mkutano wa Baraza la Madiwani la kujadili na kupitisha rasimu ya bajeti hiyo, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita Mhe. Costantine Morandi Mtani amesema bajeti hiyo imezingatia mapendezo yote muhimu ya waheshimiwa madiwani na hivyo itakwenda kutatua changamoto mbalimbali za wananchi.

Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Geita wakifuatilia Mkutano wa Baraza hilo

Akiwasilisha rasimu ya bajeti hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mji, Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu Halmashauri ya Manispaa ya Geita, Ndg. Samson Ndaro amesema Halmashauri inakadiria kupokea na kutumia jumla ya shilingi 68,393,812,906.00 kutoka katika vyanzo mbalimbali.

Ndg. Ndaro ameongezea kusema vyanzo hivyo ni mapato ya ndani shilingi bilioni 20,846,734,902.00, matumizi mengineyo (Ruzuku ya Serikali) shilingi bilioni 1,031,607,000.00, Mishahara (Ruzuku ya Serikali) shilingi bilioni 32,286,649,150.00, miradi: fedha za ndani (Ruzuku) shilingi bilioni 4,219,164,414.00, miradi: fedha za nje (Wahisani) 4,634,413,0000.00, CSR Shilingi bilioni 5,025,244,440.00 na michango ya wananchi na wadau wengine wa maendeleo shilingi milioni 350,000,000.00

Aidha, Ndg. Ndaro amesema vipaumbele vya bajeti hiyo ni kuongeza mapato ya ndani kutoka bilioni 19,965,455,000.00 ya sasa hadi bilioni 20,846,734,902.00, ili kuimarisha shughuli za utawala bora, Kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za afya, Uimarishaji wa usafi wa mazingira, Kuboresha miundombinu ya shule za Msingi, Uwezeshaji wananchi kiuchumi, Ukamilishaji wa miradi viporo, Umilikishaji wa maeneo ya umma.

Aidha Waheshimiwa Madiwani wameonesha kuwa na Imani na maono chanya katika maandalizi ya mipango na bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 ikiwemo Baraza la wafanyakazi, kamati ya ukimwi, kamati ya elimu, kamati ya uchumi, ujenzi na mazingira, kamati ya fedha, Utawala na mipango.

Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia Baraza la Madiwani

Hata hivyo katika Baraza hilo la kupitisha rasimu ya bajeti Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita Ndg. Yefred Myenzi amewapongeza Waheshimiwa Madiwani wa kata zote kwa kuwa wafuatiliaji wa miradi ya maendeleo na michango yao katika kuendeleza Halmashauri, Pia ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za kuendeleza miradi mbalimbali ikiwemo miradi ya maji, barabara, umeme, ujenzi wa shule na vituo vya Afya.

Ndg. Yefred Myenzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita akichangia hoja katika Baraza hilo

Naye, Katibu wa Wilaya wa Chama cha Mapinduzi CCM, Ndg. CDE. Michael Msuya, amewapongeza madiwani na wataalamu kuwa na umoja katika kuijenga Manispaa ya Geita, amewataka pia kushirikiana na viongozi wa ngazi ya Mitaa na Vijiji katika ukusanyaji wa mapato na waisimamie ili iweze kuwanufaisha wao na wananchi kwa ujumla.

Katibu wa Wilaya wa Chama cha Mapinduzi CCM, Ndg. CDE. Michael Msuya akichangia hoja katika Baraza hilo

Uandaji wa Mpango na rasimu ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26, umeandaliwa kwa mujibu wa Kifungu na. 21 cha sheria ya bajeti, sura 439 na kanuni zake za mwaka 2015. Maandalizi ya mpango huu wa bajeti yamezingatia ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2020 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mpango wa tatu wa maendeleo ya Taifa wa miaka mtano 2021/22 - 2025/26, malenzo ya maendeleo endelevu 2030 na maelekezo mahsusi ya serikali.

BOFYA HAPA KUSOMA TAARIFA KWA UMMA

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa