• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Nyuki na Misitu
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Sekondari Mpya Shiloleli Kuwakomboa Wanafunzi

Posted on: May 26th, 2022

Sekondari Mpya Shiloleli Kuwakomboa Wanafunzi

Kukamilika kwa ujenzi wa Shule mpya ya kwanza ya Sekondari katika kata ya Shiloleli Halmashauri ya Mji wa Geita ambayo inajengwa kupitia mradi wa SEQUIP kutoka Serikali kuu  kutawatatulia changamoto ya kutembea umbali wa kilomita 16 kwa safari moja wanafunzi wa kata hiyo ambao kwa sasa wanakwenda kupata masomo yao katika Shule ya Sekondari Bulela iliyoko kata ya Jirani.

Akizungumza na mwandishi wa Habari hii hivi karibuni, Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Bulela Mwalimu Pelicia Ponsian ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwakumbuka wanafunzi wa Shiloleli na kuona umuhimu wa kupata shule katika mazingira yao.

Mwalimu Ponsian amesema kuwa uwepo wa shule hiyo mpya utawasaidia jumla ya wanafunzi 183 wanaosoma katika shule yake wanaotoka kata ya Shiloleli ambapo wanatembea umbali mrefu na wakati mwingine hususan kipindi cha masika wanakwama kufika shuleni au kufika shule kwa kuchelewa na kukuta masomo yameshaanza kufundishwa.

Mwalimu Ponsian ameongeza kuwa  changamoto nyingine ni matokeo ya wanafunzi hao yamekuwa si ya kuridhisha kwa sababu uelewa wao darasani hupungua kutokana na uchovu wa safari ya kutoka nyumbani hadi shule, kushinda njaa, utoro wa rejareja ambao husababishwa na sababu zilizo nje ya uwezo wa wanafunzi kama uwepo wa wanyama wakali na vibaka  kwenye mapori wakati wa kwenda shuleni.

Mayala Samike, mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari Bulela ni miongoni mwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu kufika shuleni, ambaye amesema kushinda na njaa Pamoja na kukosa vipindi vya kwanza darasani imekuwa sehemu ya Maisha yao hali inayopelekea kuzorota kwa uwezo wake kitaaluma kwani wakirejea nyumbani baada ya masomo wanakuwa na uchovu ambao huwalazimu kulala na kushindwa kupata muda wa kujisomea shuleni.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Shiloleli Mhe. Boniphace Kaswahili Fulano amesema yeye ameunga mkono juhudi za Serikali kwa kutoa bure eneo lake lenye Zaidi ya ekari tisa ili shule ya Sekondari ya kwanza iweze kujengwa na kuwanufaisha Watoto wa kata hiyo. Pia ametoa wito kwa wazazi kuwahamasisha Watoto kupenda shule kwani elimu ndiyo ufunguo wa Maisha.

Shule mpya ya Sekondari katika Kata ya Shiloleli ni miongoni mwa shule mpya 11 za Sekondari zilizojengwa katika Halmashauri ya Mji Geita kwa lengo la kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani na kuwaondolea adha ya kutembea umbali mrefu kufika shule kwa baadhi ya wanafunzi wanaotumia muda mwingi kutembea mpaka shuleni kwa ajili ya masomo.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 25, 2022
  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI May 10, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Wananchi Wahimizwa Kupanda miti Ili Kutunza Mazingira

    June 23, 2022
  • Maonyesho ya Expo Dubai Yaleta Neema Geita

    June 15, 2022
  • Wakurugenzi Waagizwa Kutenga Bajeti za Madampo

    June 07, 2022
  • Wakurugenzi Waagizwa Kutenga Bajeti za Madampo

    June 07, 2022
  • Zaidi

Video

Mtakuja Inayomeremeta
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa