Halmashauri ya Manispaa ya Geita kupitia kitengo cha lishe leo tarehe 21, Novemba, 2025 imefanya hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Lishe Kitaifa iliyofanyika katika Kituo cha Afya Nyankumbu kilichopo katika Kata ya Nyankumbu, yenye kauli mbiu inayosema "AFYA NI MTAJI WAKO: ZINGATIA UNACHOKULA"
Akihutubia katika maadhimisho hayo Mganga Mkuu wa Manispaa ya Geita, Dkt. Sunday Mwakyusa amesema;
"Lengo la kufanya maadhimisho haya ni kutoa elimu ya lishe na kuhamasisha umma kuhusu faida za lishe bora na athari za utapiamlo kwa afya na maendeleo kiuchumi na kijamii."
"Ulaji usiofaa huleta utapiamlo kwa watu wote, hasa watoto chini ya miaka mitano ambao huathiri maendeleo ya ukuaji wao, uwezo wao wa kufikiri wakiwa shule na hata wakiwa watu wazima. Hali hii huepelekea kuwa na jamii isiyo na afya bora ambayo haiwezi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi katika kuleta maendeleo ya mtu momoja mmoja, jamii na taifa kwa ujumla." Aliongezea Dkt. Sunday
Aidha, Mratibu wa Lishe wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita, Ngd. Matovu Muhihi amesema, maadhimisho siku ya lishe huadhimishwa kila mwaka ili kuhamasisha umma kuhusu faida za lishe bora na athari za utapiamlo kwa afya na maendeleo kiuchumi na kijamii.
Ndg. Matovu ameongezea kusema kuwa kabla ya kufikia kilele cha maadhimisho haya, kitengo cha lishe kilitoa elimu ya lishe na kufanya upimaji wa hali ya lishe katika baadhi za shule za msingi na sekondari za serikali na binafsi, vituo vya kutolea huduma za afya vya serikali na binafsi na Kutoa elimu ya lishe kwa njia ya redio ili kuhakikisha jamii inakuwa na uelewa mzuri wa masuala muhimu ya lishe.
Wananachi wameshukuru kwa kushiriki katika elimu hii na kuahidi kuendelea kutoa Elimu ya lishe bora kwa wengine.
Geita Tanzania
Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita
Namba ya Simu: 0282520437
Mobile:
Barua pepe: td@geitatc.go.tz
Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa